Go to full page →

Kutoka kwa Kukata Tamaa na Kuelekea Uhakikisho Tumaini TSHM 166

Kwa namna kamilifu zaidi kuliko wakati wote wa mbele wanafunzi walikuwa “wamemwona, yule ambaye Musa katika sheria, na manabii, waliandika, juu yake.” Mashaka, kukata tamaa, yakatoa nafasi kwa uhakikisho, kwa imani isiyokuwa na wingu. Walipita katika jaribio kubwa lisiloawezekana na waliona namna gani neno la Mungu lilipata ushindi kwa kutimilika. Toka sasa na kuendelea nikitu gani kingeweza kutisha imani yao? Katika huzuni kali zaidi walipata “faraja yenye nguvu”, tumaini lililokuwa kama “nanga ya roho, vyote viwili kweli na kusimama imara.” Waeb. 6:18, 19. TSHM 166.5

Asema Bwana: “Watu wangu hawatapatishwa haya kamwe.” “Kilio kinakawia kwa usiku, lakini furaha asubui.” Yoeli 2:26; Zaburi 30:5. Kwa siku ya kufufuko kwake wanafunzi hawa wakakutana na Mwokozi, na mioyo yao ikawaka ndani yao walipokuwa wakisikiliza maneno yake. Kabla ya kupanda kwake, Yesu akawaagiza, “Kwendeni katika duniani pote, mukahubiri Habari Njema,” akaongeza “Na tazama, mimi ni pamoja nanyi siku zote.” Marko 16:15; Matayo 28:20. Kwa siku ya Pentekote Mufariji aliyeahidiwa akashuka, na roho za waaminifu zikasisimka na kwa kuona kuwapo kwa Bwana wao aliyepanda (mbinguni). TSHM 167.1