Go to full page →

Wenye Zambi Walimushota Kristo TSHM 26

Wavaudois walitamani sana kufungulia mioyo hizi zilizoumia na njaa ya habari za amani katika ahadi za Mungu na kuwaonyesha kwa Kristo kama tumaini lao la pekee la wokovu. Mafundisho kwamba matendo mema yanaweza kuwa pahali pa zambi yaliyotambuliwa kwa kuwa msingi wake niwa uongo. Tabia nzuri za Mwokozi aliyesulibiwa na kufufuka zinakuwa, ndiyo msingi wa imani ya kikristo. Hali ya matumaini ya moyo kwa Kristo inapaswa kuwa karibu sana kama vile kiungo kwa mwili ao cha tawi kwa mzabibu. TSHM 26.4

Mafundisho ya wapapa na wapadri yaliongoza watu kutazama Mungu na hata Kristo kama wakali na wa kugombeza, kwa hiyo bila huruma kwa mtu kwamba uombezi wa wapadri na watakatifu ulipaswa kuombwa. Wale ambao akili zao zimeangaziwa walitamani sana kuondoa vizuizi ambavyo Shetani amevijaza, ili watu waweze kuja mara moja kwa Mungu, kuungama zambi zao, na kupokea msamaha na amani. TSHM 26.5