Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents
Tangu Sasa Hata Milele - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    “Wakati Umetimia”

    Kristo aliwatuma na ujumbe: “Wakati umetimia, ufalme wa Mungu ni karibu. Tubuni mukaamini Habari Njema.” Marko 1:15. Ujumbe ule ulikuwa na msingi katika unabii wa Danieli 9. ‘’Majuma makumi sita na tisa” yalipashwa kufikia kwa Mfalme na wanafunzi walitazamia mbele kuimarishwa kwa ufalme wa Masiya kule Yerusalema ili atawale juu ya dunia yote nzima.TSHM 165.1

    Wakahubiri habari iliyotolewa kwao, ingawa walikosa kufahamu maana yake. Wakati matangazo yao msingi wake ulikuwa katika Danieli 9:25, hawakuona katika shairi lililofuata kwamba Masiya alipashwa “kukatiliwa mbali.” Mioyo yao ilikuwa juu ya utukufu wa utawala wa kidunia; jambo hili likapofusha akili yao.TSHM 165.2

    Kwa wakati kabisa walipotumainia kuona Bwana wao kupanda kwa kiti enzi cha Dawidi, walimwona akikatwa, kupigwa, kuzihakiwa, na kuhukumiwa juu ya msalaba. Kukata tamaa kwa namna gani na uchungu yaliumiza mioyo ya wale wanafunzi!TSHM 165.3

    Kristo alikuja kwa wakati halisi uliotabiriwa. Maandiko yalitimia katika habari yote. Neno na Roho wa Mungu ilishuhudia agizo la Mwana wake. Lakini mafikara ya wanafunzi yalifunikwa na mashaka. Kama Yesu alikuwa Masiya wa kweli wangetumbukia katika sikitiko na uchungu? Hili ndilo swali lililotesa roho zao wakati wa saa za kukata tamaa za Sabato ile iliyokuwa katikati ya kifo chake nakufufuka kwake.TSHM 165.4

    Lakini hawakuachwa. “Nikikaa katika giza, Bwana atakuwa nuru kwangu... Atanileta inje kwa nuru na nitatazama haki yake.” “Kwa wenye haki nuru inangaa gizani.” “Nitafanya giza kuwa nuru mbele yao; na pahali pa kupotoka patanyoshwa. Maneno haya nitawafanyia, wala sitawaacha.” Mika 7:8, 9; Zaburi 112:4; Isaya 42:16.TSHM 165.5

    Matangazo yaliyofanywa na wanafunzi yalikuwa halisi “Wakati umetimia, ufalme wa Mungu ni karibu.” “Kwa mwisho wa wakati” majuma makumi sita na tisa ya Danieli 9 ambayo yalipashwa kufikia kwa Masiya, “Mupakaliwa”--Kristo alipokea mafuta ya Roho baada ya ubatizo wake kwa Yoane. “Ufalme wa Mungu” haikuwa, kama walivyofundishwa kuamini, ufalme wa kidunia. Wala ule ujao, ufalme wa milele ambao “na wote wenye mamlaka watamutumikia na kumutii.” Danieli 7:27.TSHM 165.6

    Neno hili “Ufalme wa Mungu” linatumiwa kutaja mambo yote mawili ufalme wa neema na ufalme wa utukufu Mtume anasema: “Basi, tukaribie kiti cha neema pasipo woga,” ili tupate huruma na kuona neema. Waebrania 4:16. Kuwako kwa kiti cha ufalme kunaonyesha kuwako kwa ufalme. Kristo anatumia neno la “Ufalme wa mbinguni” kutaja kazi ya neema juu ya mioyo ya watu. Kwa hiyo kiti cha utukufu kinaonyesha ufalme wa utukufu. Matayo 25:31, 32. Ufalme huu ukingali wa wakati ujao. Hautasimamishwa hata wakati wa kuja kwa Kristo mara ya pili.TSHM 165.7

    Wakati Mwokozi alipotoa maisha yake na akalia kwa sauti kubwa, “imekwisha,” ahadi ya wokovu iliyo fanywa kwa mme na mke wenye zambi katika Edeni ikatimilika. Ufalme wa neema, ambao ulikuwako mbele kwa ahadi ya Mungu, ukaimarishwa.TSHM 166.1

    Kwa hiyo kifo cha Kristo jambo ambalo wanafunzi walitazamia kama maangamizi ya tumaini lao ilikuwa ni milele kwa kweli. Wakati ilileta uchungu mkali, ilikuwa ushahidi kwamba imani yao ilikuwa halisi. Jambo lililowatumbukiza katika kukata tamaa likafungua mlango wa tumaini kwa waaminifu wote wa Mungu katika vizazi vyote.TSHM 166.2

    Zahabu safi ya upendo wa wanafunzi kwa ajili ya Yesu ilichanganyika na msingi wa tamaa mbaya ya choyo. Maono yao yalivutwa na kiti cha ufalme, taji, na utukufu. Kiburi chao cha moyo, kiu cha utukufu wa kidunia, vikawaongoza kupita bila kujali maneno ya Mwokozi ya kuonyesha asili ya kweli ya ufalme wake, na kuonyesha zaidi kifo chake. Makosa haya yaliishia kwa jaribio ambalo liliruhusiwa kwa ajili ya kusahihishwa kwao. Kwa wanafunzi ilikuwa ni kutolewa Habari Njema ya utukufu ya Bwana wao aliyefufuka. Kuwatayarisha kwa kazi hii, maarifa ambayo yalionekana machungu sana yaliruhusiwa.TSHM 166.3

    Baada ya kufufuka kwake Yesu akajionyeshea kwa wanafunzi wake njiani kwenda Emausi, na, “akawaelezea maana ya maneno yote yaliyo andikwa juu yake.” Ilikuwa kusudi lake kukaza imani yao juu ya “neno la kweli la unabii.” (Luka 24:27; 2 Petro 1:19). Si kwa ushuhuda wake mwenyewe tu, bali kwa mambo ya unabii wa Agano la Kale. Na kama hatua ya kwanza kabisa katika kutoa maarifa haya, Yesu akaongoza wanafunzi kwa “Musa na manabii wote” wa Maandiko ya Agano la Kale.TSHM 166.4

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents