Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents
Tangu Sasa Hata Milele - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    Safari za Kwanza kutoka kwa Habari Njema

    Namna gani kanisa lilitoka mara ya kwanza kwa unyenyekevu wa habari njema? Kwa njia ya kupatana na kipagani, ili wapagani wakubali wepesi dini ya kikristo. “Karibu kufikia mwisho wa kumalizia karne ya pili karibu makanisa mengi yalikubali sura mpya... Kama wanafunzi wa zamani walipopumzika katika makaburi yao, watoto wao pamoja na waliogeuka wapya, ... wakaendelea mbele na kutoa mfano mpya kwa dini.” “Wingi wa wapagani, kujaa katika kanisa, kuchukua pamoja nao desturi zao, tamaa, na ibada ya sanamu.” Dini ya Kikristo ikategemea mapendeleo na usaada wa watawala wa dunia. Ikakubaliwa kwa jina tu na wengi. “Lakini wengi wakadumu katika mambo ya kipagani, zaidi kuabudu kwa uficho sanamu zao.”TSHM 185.3

    Je, matendo ya namna ile haikufanyika karibu katika kila kanisa linalojiita lenyewe Protestanti? Kwa namna wenye kulianzisha waliokuwa na roho ya kweli ya matengenezo walikufa, wazao wao wakatoa mfano mpya.” Kukataa kwa upofu kukubali kweli yo yote mbele ya yale wababa zao waliona, watoto wa watengenezaji wakatoka kwa mfano wao wa kujinyima na kuacha dunia.TSHM 185.4

    Aa, kwa wingi wa namna gani makanisa ya watu wengi yalitoka kwa kanuni ya Biblia! Akazungumzia juu ya pesa, John Wesley akasema: ” Usipoteze sehemu ya talenta hii ya damani kwa kupamba nyumba yako na vyombo vya ufundi; katika mapicha ya bei kali, kupamba... Wakati wote utakapovaa mavazi ya rangi ya zambarau nyekundu na kitani,’ na zaidi` kuwa na maisha ya anasa kila siku,’ bila shaka wengi watashangilia uzuri wa tamaa yako, kwa ukarimu wako na utu wema wako. Lakini utoshelewe zaidi na heshima itokayo kwa Mungu.”TSHM 185.5

    Watawala, watu wa siasa, wanacheria, waganga, wachuuzi, wanajiunga kanisani kwa kusudi la kwendesha faida zao za kidunia. Makundi mbalimbali ya dini, yakaja kusaidiwa na utajiri wa hawa wakidunia waliobatizwa, kuwa njia nzuri sana ya kuvuta watu wengi. Makanisa mazuri sana, na garama nyingi yakajengwa. Mshahara wa juu sana ulilipwa kwa mchungaji mwenye kipawa cha kukaribisha watu. Mahubiri yake yalipaswa kuwa rahisi na kupendeza kwa masikio ya siku hizi. Kwa hiyo zambi za siku hizi zinafichwa chini ya hila za wema, mfano wakuogopa Mungu.TSHM 185.6

    Mwandishi mmoja katika New York Independent akasema hivi juu ya dini ya Methodiste kama inavyokuwa: “Msitari wa mtengano kati ya wanaomwogopa Mungu na waovu unapotea katika namna ya kivuli, na watu wa bidii kwa pande zote mbili hujitahidi kutupia mbali tofauti yote kati ya desturi zao za kutenda na furaha.”TSHM 186.1

    Katika mwendo huu wa kutafuta anasa, kujinyima kwa ajili ya Kristo karibu kulipotea kabisa. “Kama feza zinahitajiwa sasa, ... hakuna mtu anayepashwa kuitwa kwa kutoa. Aa hapana! kutayarisha maonyesho ya biashara, michezo ya kuingiza picha, michezo ya bahati (loterie), chakula cha jioni (banquet), wala kitu cha kula--kila kitu cho chote kwa kupendeza watu.”TSHM 186.2

    Robert Atkins anaonyesha picha ya upungufu wa kiroho katika Uingereza: ‘’ Uasi, uasi, uasi, tazama neno lililochorwa mbele ya makanisa yote; na wangejua, na waliiisikia na kungekuwa na tumaini; lakini, ole! Wakalalamika: “Sisi ni tajiri, tumepata vitu vingi; wala hatuhitaji kitu chochote.”‘ Zambi kubwa iliyoshitakiwa Babeli ni kwamba “amefanya mataifa yote kunywa mvinyo ya gazabu ya uasherati wake. “Kikombe hiki ni mfano wa mafundisho ya uongo yale aliyokubali kama matokeo ya urafiki pamoja na dunia. Kwa nafasi yake hutumia mvuto wa uovu juu ya dunia kwa kufundisha mafundisho yaliyopinga maneno wazi ya Biblia.TSHM 186.3

    Kama haingekuwa kwamba dunia inaleweshwa na mvinyo wa Babeli, wengi wangalisadikishwa na kungeuzwa kweli kamili za Neno la Mungu. Lakini imani ya dini inaonekana kuwa na machafuko sana na kutopatana hata watu hawaujui kitu gani cha kuamini. Zambi ya dunia isiyotubiwa inalala mlangoni mwa kanisa.TSHM 186.4

    Ujumbe wa malaika wa pili haukutmilika katika mwaka 1844. Makanisa basi yalianguka kiroho kwa kukataa nuru ya ujumbe wa kurudi kwa Yesu, lakini hayakuanguka kabisa. Namna walikuwa wakiendelea kukataa mambo ya ukweli wa pekee kwa ajili ya wakati huu waliendelea kuanguka chini na kuendelea chini. Bado, lakini, itawezekana kusemwa kwamba “Babeli imeanguka, ... kwa sababu amefanya mataifa yote kunywa mvinyo wa hasira ya uasherati wake.” Makanisa ya Kiprotestanti yanakuwa ndani ya masitaka ya malaika wa pili. Lakini kazi ya uasi haijafikia hatua yake ya mwisho.TSHM 186.5

    Mbele ya kuja kwa Bwana, Shetani atatumika “na uwezo wote, na ishara na maajabu ya uwongo, na udanganyifu wote wa uzalimu”; na wale ambao “hawakupokea mapendo kwa kweli, wapate kuokolewa,” wataachwa kupokea “nguvu ya upotevu, hata waamini uwongo.” 2 Watesalonika 2:9-11. Hata muungano wa kanisa pamoja na dunia utakapotimia kabisa ndipo kuanguka kwa Babeli kutakuwa kamili. Mabadiliko ni ya kidogo kidogo na kutimilika kamili kwa Ufunuo 14:8 kunakuwa kwa wakati ujao.TSHM 187.1

    Bila kutazama giza ya kiroho inayokuwa katika makanisa yanaosimamisha Babeli, wengi wa wanafunzi wa kweli wa Kristo wangali wanapatikana katika ushirika wao. Wengi hawajaona kamwe kweli za kipekee kwa ajili ya wakati huu. Wengi ni wale wanaotamani nuru kamili zaidi. Wanatazama bila kuona sura ya Kristo katika makanisa ambamo wanaambatana nayo.TSHM 187.2

    Ufunuo 18 huonyesha wakati ambao watu wa Mungu ambao wakingali katika Babeli wataitwa kujitenga kwa ushirika wake. Ujumbe huu, wa mwisho unaopaswa kutolewa kwa dunia, itatenda kazi yake. Nuru ya kweli itaangaza juu ya wote ambao mioyo yao inafunguliwa kwa kuipokea, na wana wote wa Bwana wanaokuwa katika Babeli watasikia mwito: “Tokeni kwake, watu wangu.” Ufunuo 18:4.TSHM 187.3

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents