Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents
Tangu Sasa Hata Milele - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    Kazi ya Hukumu

    Katika agano jipya zambi za mwenye kutubu zinawekwa kwa imani juu ya Kristo na kuhamishwa kweli kwa Pahali patakatifu pa mbinguni. Na kama kusafishwa kwa mfano kwa Pahali patakatifu pa kudunia kulifanywa na ondoleo la zambi ambazo zilipachafua, vivyo hivyo utakaso wa sasa wa mbinguni unatimizwa kwa ondoleo, ao kufutwa, kwa zambi zilizoandikwa pale. Lakini kabla ya jambo hili kuweza kufanyika uchunguzi unapashwa kufanyika pale wa vitabu vya ukumbusho kuonyesha ni wanani, kwa njia ya toba na imani katika Kristo, wanaostahili kupata faida ya upatanisho wake. Basi utakaso wa Pahali patakatifu kwa hivi unahusika na kazi ya uchunguzi -kazi ya hukumu -ya kutangulia kuja kwa Kristo, kwa maana wakati atakuja, na mushahara wake ni pamoja naye kulipa kila mutu kama ilivyo kazi yake. Ufunuo 22:12.TSHM 203.1

    Kwa hivyo wale waliofuata nuru ya neno la unabii waliona kwamba, badala ya kuja duniani kwa mwisho wa siku 2300 katika mwaka 1844, Kristo aliingia kwa Pahali patakatifu pa patakatifu mno pa mbinguni kufanya kazi ya mwisho ya upatanisho wa kutangulia kuja kwake.TSHM 203.2

    Wakati Kristo katika uwezo wa damu yake anapoondoa zambi za watu wake kutoka kwa Pahali patakatifu pa mbinguni kwa mwisho wa huduma yake, ataziweka juu ya Shetani, anayepashwa kupata azabu ya mwisho. Mbuzi wa Azazeli akatumwa mbali katika inchi isiyokaliwa, hawezi kuja tena katika makutano ya Waisraeli. Ndivyo Shetani atakavyoangamizwa milele mbele ya Mungu na watu wake, na ataondolewa maisha katika uharibifu wa mwisho wa zambi na wenye zambi.TSHM 203.3

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents