Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents
Tangu Sasa Hata Milele - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    Kufukuziwa Mbali Kutoka Mbinguni

    Shetani na jeshi lake wakatupa laumu la uasi wao juu ya Kristo; kama hawakulaumiwa, kama hawangeasi kamwe. Wagumu na wakiburi, huku wakajitangaza kwa matukano kuwa watu wasiokuwa na kosa na kwamba waliteswa na mamlaka makali. Muasi mkubwa wa waliomfuata wakafukuzwa kutoka mbinguni. Tazama Ufunuo 12:7-9.TSHM 243.2

    Roho ya Shetani ingali inaendesha uasi duniani katika wana wa uasi. Kama yeye wakaahidia watu uhuru kwa kuvunja sheria ya Mungu. Hakikisho la zambi likaendelea kuamsha uchuki. Shetani anaongoza watu kujihakikisha wao wenyewe na kutafuta huruma ya wengine katika zambi zao. Badala ya kusahihisha makosa yao, wanaamsha hasira juu ya mwenye kukaripia, kama kwamba wanakuwa chanzo cha shida. Kwa kusingizia kwa namna ileile ya tabia ya Mungu kama alivyoyatumia mbinguni, kumfanya kuwa kama mwenye kuzaniwa kama mkali na wa kushurutisha, Shetani akashawishi mtu kwa zambi. Akatangaza kwamba vizuizi visivyo na haki vya Mungu viliongoza kuanguka kwa mtu, kama vilivyoongoza kwa uasi wake mwenyewe.TSHM 243.3

    Katika kufukuziwa kwa Shetani kutoka mbinguni, Mungu alitangaza haki yake na heshima. Lakini wakati mtu alipotenda zambi, Mungu alitoa ushuhuda wa upendo wake kwa kutoa Mwana wake kufa kwa ajili ya taifa lililoanguka. Katika upatanisho tabia ya Mungu imefunuliwa. Mabishanomakubwa ya msalaba yanaonyesha kwamba zambi haikuwa na hekima yo yote kulipizwa juu ya utawala wa Mungu. Wakati wa huduma ya kidunia ya Mwokozi, mdanganyi mkubwa akafunuliwa. Matukano ya wazi ya kutaka kwamba Kristo amupe heshima kuu, uovu usiolala uliomuwinda pahali po pote, kuongoza mioyo ya makuhani na watu kukataa upendo wake na kulalamika kwa sauti, “Asulibiwe! asulibiwe!” --yote haya yaliamsha mshangao na hasira ya ulimwengu. Mfalme wa zambi akatumia uwezo wake wote na werevu kuharibu Yesu. Shetani akatumia watu kama wajumbe wake kujaza maisha ya Mwokozi kwa mateso na huzuni. Chuki na wivu na uovu, machukio na kisasi, vikaanguka kutoka Kalvari juu ya Mwana wa Mungu.TSHM 243.4

    Sasa kosa la Shetani likaonekana wazi. Alifunua tabia yake ya kweli. Mashitaki ya uwongo ya Shetani juu ya tabia ya Mungu yakaonekana katika nuru yao ya kweli. Alimshitaki Mungu juu ya kutafuta kujiinua mwenyewe katika kuomba utii kwa viumbe vyake na akatangaza kwamba wakati Muumba alipolazimisha wote kujikana mwenyewe, Yeye mwenyewe hakutumia kujikana mwenyewe na hakutoa kafara yo yote. Sasa ilionekana kwamba Mtawala wa ulimwengu alitoa kafara kubwa sana ambayo upendo uliweza kufanya, “maana, Mungu alikuwa ndani ya Kristo, akipatanisha ulimwengu naye mwenyewe.” 2 Wakorinto 5:19. Kusudi aharibu zambi Kristo akajinyenyekea mwenyewe na kuwa mtiifu hata mauti.TSHM 244.1

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents