Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents
Tangu Sasa Hata Milele - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    Malaika Walinzi

    Malaika mlinzi amewekwa kwa kila mfuasi wa Kristo. “Malaika ya Bwana anapiga kambi kuzunguka wale wanaomwogopa, na anawaokoa.” Akasema Mwokozi, juu ya wale wanaomwamini: “Mbinguni malaika zao wanatazama siku zote uso wa Baba yangu.” Zaburi 34:7; Matayo 18:10. Watu wa Mungu, walihatarishwa kwa uovu usiolala wa mfalme wa giza, wanaahidiwa na ulinzi usiokoma wa malaika. Matumaini ya namna hiyo yanatolewa kwa sababu kunakuwa na nguvu kubwa za uovu za kukutana nazo--nguvu zisizohesabika, imara na zisizochoka.TSHM 250.1

    Pepo wachafu, kwa mwanzo waliumbwa pasipo zambi, walikuwa sawasawa kwa tabia, uwezo, na utukufu pamoja na viumbe vitakatifu vile vinavyokuwa sasa wajumbe wa Mungu. Lakini walipoanguka katika zambi, wanashiriki pamoja kwa kufezeresha Mungu na uharibifu wa watu. Kwa kuungana pamoja na Shetani katika uasi, wanashirikiana katika vita kupigana na mamlaka ya Mungu.TSHM 250.2

    Historia ya Agano la Kale inataja kuwapo kwao, lakini kwa wakati Yesu alipokuwa duniani pepo wachafu wakaonyesha uwezo wao kwa namna ya ajabu sana. Kristo alikuja kwa ajili ya ukombozi wa mtu, na Shetani akakusudia kutawala ulimwengu. Akafanikiwa katika kuimarisha ibada ya sanamu katika kila upande wa dunia isipokuwa Palestina. Kwa inchi ile tu ambayo haikujitoa kamili kwa mshawishi, Yesu akakuja, kunyosha mikono yake ya upendo, kualika wote kupata msamaha na amani kwake. Majeshi ya giza yakafahamu kwamba kama kazi ya Kristo inapata ushindi, mamlaka yao ingekuwa karibu kumalizika.TSHM 250.3

    Kwamba watu wamekuwa na pepo mbaya inasemwa wazi katika Agano Jipya. Kwa hivi watu walioteswa si kwa sababu tu ya magonjwa ya kawaida; Kristo alifahamu kuwako kwa chanzo cha magonjwa na nguvu ya pepo wachafu. Wenye pepo wachafu kule Gadara, wenye wazimu wa hali mbaya, kujinyonga, kujitapa, kutosha povu, kukasirika, walikuwa wakijitesa wao wenyewe na kuhatarisha wote waliopaswa kuwakaribia. Kutokwa kwao kwa damu, kukabadili hali ya mwili na mawazo yenye kuhangaika yalionyesha ajabu ya kufurahisha sana mfalme wa giza. Mumojawapo wa pepo wachafu wakutawala wanaoteswa akatangaza, “Jina langu ni Legioni: maana: Jeshi.” Marko 5:9. Katika jeshi la Roma legioni ilikuwa ya kuanzia watu elfu tatu hata elfu tano. Kwa agizo la Yesu pepo wachafu wakatoka kwa watu wao waliokuwa wanatesa, kuwaacha wanapotu- lia, wenye akili, na wapole. Lakini pepo wachafu wakarusha kundi la nguruwe katika bahari, na kwa wakaaji wa Gadara hasara kubwa ikazima mibaraka Kristo aliyoitoa; mponya wa Mungu akalazimishwa kutoka. Tazama Matayo 8:22-34. Kwa kulaumu hasara yao juu ya Yesu, Shetani akaamsha choyo cha woga kwa watu na kuwakataza kusikiliza maneno yake.TSHM 250.4

    Kristo akaruhusu pepo wachafu kuangamiza nguruwe kama laumu kwa Wayuda waliolea wanyama najisi kwa ajili ya faida. Kama Kristo hakuzuia pepo wachafu, wangalitumbukiza si nguruwe tu, bali wachungaji wao pia na wenye nguruwe ndani ya bahari.TSHM 251.1

    Tena, jambo hili liliruhusiwa ili wanafunzi waweze kushuhudia uwezo mkali wa Shetani juu ya wote wawili mtu na mnyama, ili wasiweze kudanganywa kwa mipango yake. Ilikuwa vilevile mapenzi yake kwamba watu walipashwa kutazama uwezo wake kuvunja utumwa wa Shetani na kufungua wafungwa wake. Ingawa Yesu Mwenyewe alitoka, watu waliookolewa kwa ajabu sana wakaendelea kutangaza rehema ya Mkarimu wao.TSHM 251.2

    Mifano mingine imeandikwa: Binti wamwanamuke wa Sirofoinike, aliyesumbuliwa vikali kwa Shetani, ambaye Yesu alifukuza kwa neno lake (Marko 7:26-30); kijana aliyekuwa na pepo ambayo mara kwa mara “kumtupa katika moto, na katika maji, amwangamize.” (Marko 9:17-27); mwenye pepo, aliyeteswa na pepo ya ibilisi mchafu aliyechafua Sabato tulivu kule Kapernaumu (Luka 4:33-36)--wote waliponyeshwa kwa Mwokozi. Karibu kila mfano, Kristo akasema pepo mchafu kama kitu chenye akili, kumwagiza kutotesa mtu wake tena. Waabuduo kule Kapernaumu “wote wakashangaa sana, wakasemezana wao wenyewe wakisema: Neno gani hili; kwani kwa mamlaka na uwezo anaamuru pepo wachafu, nao wanatoka.” Luka 4:36.TSHM 251.3

    Kwa ajili ya kupata uwezo wa ajabu, wengine wakakaribisha mvuto wa Shetani. Mambo haya bila shaka hayakuwa na ugomvi pamoja na pepo wachafu. Kwa kundi hili kulikuwa wale waliokuwa na pepo ya uaguzi--Simon Magus, Elima mchawi yule, na kijakazi mwenye pepo aliyefuata Paulo na Sila kule Filipi. Tazama Matendo 8:9,18; 13:8; 16:16-18.TSHM 251.4

    Hakuna wanaokuwa katika hatari kubwa kuliko wale wanaokana kuwako kwa Shetani na malaika zake. Wengi wanajali mashauri yao wanapoona wao wenyewe kuwa wakifuata hekima yao wenyewe. Kwa namna tunavyokaribia mwisho wa wakati, wakati Shetani anapashwa kutumika kwa uwezo mkubwa kudanganya, anaeneza mahali pote imani kwamba yeye hakuwako. Ni kanuni yake kujificha mwenyewe na namna yake ya kutumika.TSHM 251.5

    Mwongo mkubwa anaogopa kwamba tutakuwa wenye kutambua mipango yake. Kwa kuficha tabia yake ya kweli akajifanya mwenyewe aonyeshwe kama kitu cha kuchekelea ao cha kuzarau. Anapendezwa kufafanishwa kama mwenye kuchekesha, mwenye msiba, nusu mnyama na nusu mwanadamu. Anapendezwa kusikia jina lake linapotumiwa katika mchezo na kicheko. Kwa sababu amejificha mwenyewe na akili kamili, swali linaulizwa sana popote: “Je, kiumbe cha namna hii kinakuwako kweli?” Ni kwa sababu Shetani anaweza kwa upesi kutawala mawazo ya wale wanaokuwa bila kufahamu mvuto wake kwamba Neno la Mungu linafungua mbele yetu nguvu za siri yake, kwa hivi kutuweka kwa angalisho.TSHM 252.1

    Tunaweza kupata kimbilio na wokovu katika uwezo mukubwa wa Mkombozi wetu. Tunachunga vizuri sana nyumba zetu kwa mapingo na kufuli kulinda mali yetu na maisha kwa watu waovu, lakini ni marahaba kufikiri juu ya malaika waovu kushindana na mashambulio yake tunayokuwa nayo, katika nguvu zetu wenyewe, hakuna ulinzi. Kama wakiruhusiwa, wanaweza kuvuta mioyo yetu, kutesa miili yetu, kuharibu mali yetu na maisha yetu. Lakini wale wanaomfuata Kristo wanakuwa salama chini ya ulinzi wake. Malaika wanaopita katika nguvu wanatumwa kuwalinda. Waovu hawawezi kuvunja ulinzi aliyoweka Mungu kwa ajili ya watu wake.TSHM 252.2

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents