Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents
Tangu Sasa Hata Milele - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    33 / NI KITU GANI KINACHOLALA NG’AMBO YA PILI YA KABURI

    Shetani aliyechochea uasi huko mbinguni, alitaka kushawishi wakaaji wa dunia kuungana katika vita yake ya kumpinga Mungu. Adamu na Hawa walikuwa na furaha kamili katika utii kwa sheria ya Mungu--ushuhuda wa daima wa kupinga madai ya Shetani ulioweka mbele katika mbingu ya kuwa sheria ya Mungu ilikuwa ya taabu. Shetani akakusudia kuanzisha maanguko yao, ili aweze kumiliki dunia na hapa kuimarisha ufalme wake kwa kupingana na Aliye Juu.TSHM 260.1

    Adamu na Hawa walikuwa wakionywa juu ya adui wa hatari huyu, lakini alikuwa akitumika katika giza, kuficha kusudi lake. Kutumia nyoka kama chombo chake, ndipo kiumbe cha mfano wa kupendeza, akamwambia Hawa: “Ndiyo, Mungu amesema: Msile ya miti yote ya shamba?” Hawa akajihatarisha (akasubutu) kusemana naye na akaanguka mateka kwa uongo wake: “Mwanamuke akamwambia nyoka: Matunda ya miti ya shamba tunaweza kula; lakini matunda ya mti ulio katikati ya shamba Mungu amesema: Musile matunda yake wala musiyaguse, musife. Na nyoka akamwambia mwanamuke; Hakika hamutakufa, kwani Mungu anajua ya kama siku mutakapokula matunda yake, macho yenu yatafunguliwa, na mutakuwa kama miungu, mukijua uzuri na ubaya.” Mwanzo 3:1-5.TSHM 260.2

    Hawa akakubali, na kwa mvuto wake (mwanamuke) Adamu akaongozwa katika zambi. Wakakubali maneno ya nyoka; wakaonyesha kutotumaini Muumba wao na kuwaza ya kama alikuwa akizuia uhuru wao.TSHM 260.3

    Lakini ni kitu gani Adamu alichopata kujua kuwa maana ya maneno, “Kwa maana siku utakapokula, hakika utakufa”? Je, alipaswa kuongozwa katika maisha ya kujiinua zaidi? Adamu hakuona jambo hili kuwa maana ya hukumu ya Mungu. Mungu alitangaza ile kama azabu kwa ajili ya zambi yake, mtu alipashwa kurudi kwa mavumbi: “Kwa sababu mavumbi wewe, na utarudi kwa mavumbi.” Mwanzo 3:19. Maneno ya Shetani, “Macho yenu yatafunguliwa,” yalionekana kuwa ya kweli katika maana hii tu: macho yao yakafunguliwa kutambua ujinga wao. Wakajua ubaya na kuonja tunda la uchungu wa uasi.TSHM 260.4

    Mti wa uzima ulikuwa na uwezo wa kudumisha uzima. Adamu angeendelea kufurahia ruhusa ya uhuru wa kukaribia mti huu na kuishi milele, lakini wakati alipofanya zambi akazuiwa kwa mti wa uzima na akastahili kifo. Kufa ikaondoa kutokufa. Pale hapangaliku- wa na tumaini kwa uzao ulioanguka kama Mungu, kwa kafara ya Mwana wake, hangeleta kutokufa karibu nao. Na hivi ‘’kufa kulikuja juu ya watu wote, kwa sababu wote wamefanya zambi,” Kristo “ameleta uzima na maisha yasiyokoma nuru ni kwa njia ya Habari Njema.” Katika Kristo tu kutokufa kunaweza kupatikana. “Anayeamini Mwana ana uzima wa milele; na asiyemwamini Mwana hataona uzima.” Waroma 5:12; 2 Timoteo 1:10; Yoane 3:36.TSHM 260.5

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents