Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents
Tumaini Kuu - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    Berquin Achomwa Moto

    Kwenye nguzo ile Berquin alijitahidi kuwahutubia watu kwa maneno machache, lakini watawa walianza kupiga kelele huku askari wakigonganisha silaha zao na makelele yao yaliifunika sauti ya mfia dini. Hivyo mnamo mwaka 1529 mamlaka ya juu zaidi ya kanisa katika utamaduni wa Kifaransa, iliweka mbele ya umati wa watu waliokuwepo mwaka 1793 “kielelezo cha msingi cha kukabwa kwenye jukwaa la kunyongea maneno matakatifu ya yule anayekufa” 136Wylie, bk. 13, ch. 9. Berquin alinyongwa na mwili wake kuteketezwa kwa moto.TK 140.4

    Walimu wa imani ya matengenezo waliondoka na kwenda kwenye maeneo mengine. Lefevre alikwenda Ujerumani. Farel alirudi kusambaza nuru kwenye eneo alilokulia na mji wa kwao kule mashariki mwa Ufaransa. Ukweli aliokuwa anafundisha ulipata wasikilizaji. Alifukuzwa kutoka katika mji huo muda mfupi baadaye. Alikuwa anapita huku na huko katika vijiji akifundisha kwa siri kwenye makazi ya watu na kwenye maeneo ya maficho, akijihifadhi kwenye misitu na mapangoni kwenye sehemu alizokuwa akienda mara kwa mara alipokuwa mvulana.TK 141.1

    Kama ilivyokuwa nyakati za mitume, mateso “yalikuwa yanasaidia tu kusambaza Injili.” Wafilipi 1:12. Walipofukuzwa kutoka Paris na Meaux, “...wale waliotawanyika wakaenda huko na huko wakilihubiri neno.” Matendo 8:4. Hivyo ndivyo nuru ilivyokuwa inapenya kwenye majimbo mbalimbali nchini Ufaransa.TK 141.2

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents