Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents
Tangu Sasa Hata Milele - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    Mwito kwa Kuamka

    Kwa maoni ya siku ile kubwa Neno la Mungu linaita watu wake kutafuta uso wake katika toba:TSHM 146.1

    “Siku ya Bwana inakuja, kwani imekaribia.” “Takaseni kufunga chakula, iteni kusanyiko la dini; kusanyeni watu, takaseni makutano, kusanyeni wazee, kusanyeni watoto: ... Makuhani, watumishi wa Bwana, lia katikati ya baraza na mazabahu.” “Geukeni kwangu na moyo wenu wote, na pamoja na kufunga chakula, na kutoa machozi na kuomboleza; na pasueni moyo wenu, wala si mavazi yenu, geukeni kwa Bwana, Mungu wenu; kwa kuwa ni mwenye neema na, anayejaa huruma, si mwepesi kwa kukasirika, na mwenye rehema nyingi.” Yoeli 2:1, 15-17, 12,13.TSHM 146.2

    Kwa kutayarisha watu kusimama kwa siku ya Mungu, kazi kubwa ya matengenezo ilipashwa kutimilika. Katika huruma zake alikuwa karibu kutuma mjumbe kwa kuamsha waliojidai kuwa watu wake na kuwaongoza kujitayarisha kwa kuja kwa Bwana.TSHM 146.3

    Onyo hili linaonyeshwa katika Ufunuo 14. Hapa kunakuwa na namna tatu ya ujumbe unaoonyeshwa kama unatangazwa na viumbe vya mbinguni na mara moja ukafuatwa na kuja kwa Mwana wa mtu kwa kuvuna “mavuno ya dunia.” Nabii aliona malaika akiruka “katikati ya mbingu, mwenye Habari Njema ya milele, awahubiri wale wanaokaa juu ya dunia, na kila taifa na kabila na lugha na jamaa, akasema kwa sauti kubwa: Ogopeni Mungu, na kumutukuza kwa maana saa ya hukumu yake imekuja. Mukamwabudu yeye aliyezifanya mbingu na dunia na bahari na chemchemi za maji.” Ufunuo 14:6. 7.TSHM 146.4

    Ujumbe huu ni sehemu ya “Habari Njema ya milele.” Kazi ya kuhubiri ilipewa wala kuaminishwa kwa watu. Malaika watakatifu huongoza, lakini tangazo la sasa la habari njema linafanywa na watumishi wa Kristo duniani. Watu waaminifu, watiifu kwa maongozi ya Roho wa Mungu na mafundisho ya Neno lake, walipashwa kutangaza onyo hili. Walikuwa wakitafuta maarifa ya Mungu, kuihesabu “vema kuliko biashara ya feza, na faida yake ni nyororo kuliko zahabu safi.” “Siri ya Bwana ni pamoja nao wanaomwogopa; Naye atawaonyesha agano lake.” Mezali 3:14; Zaburi 25:14.TSHM 146.5

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents