Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents
Tangu Sasa Hata Milele - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    Uhamisho wa Shetani

    Sasa matukio yamefanyika yaliyoonyesha mbele heshima ya kazi ya mwisho kwa Siku ya upatanisho. Wakati zambi za Israeli zilipoondolewa kutoka Pahali patakatifu kwa uwezo wa damu ya sadaka ya zambi, mbuzi wa Azazeli alionyeshwa hai mbele ya Bwana. Kuhani mkuu akaungama juu yake “maovu yote ya wana wa Israeli,... kuyaweka juu ya kichwa cha mbuzi”. Walawi 16:21. Vilevile, wakati kazi ya upatanisho katika Pahali patakatifu pa mbinguni itakapotimia, ndipo, mbele ya Mungu na malaika wa mbinguni na jeshi la waliookolewa, zambi za watu wa Mungu zitawekwa juu ya Shetani; atatangazwa kuwa na kosa ya uovu wote aliolazimisha wao kuufanya. Kama vile mbuzi wa Azazeli aliochukuliwa katika inchi isiyokaliwa na watu, vivyo hivyo Shetani atahamishwa kwa dunia yenye ukiwa.TSHM 320.2

    Baada ya kuonyesha mambo ya ajabu ya kuja kwa Bwana, mfunuaji anaendelea: “kisha nikaona malaika akishuka toka mbingu, mwenye ufunguo wa shimo lisilo na mwisho, na munyororo mkubwa katika mkono wake. Akamshika yule joka mkubwa, yule nyoka ya zamani, anayeitwa Diabolo na Shetani, akamufunga miaka elfu, na akamutupa katika shimo lisilo na mwisho, na kumufunga, na kutia muhuri juu yake, asipate kudanganya mataifa tena, hata ile miaka elfu itimie; na nyuma ya hayo inapashwa afunguliwe wakati kidogo”. Ufunuo 20:1-3.TSHM 320.3

    “Shimo lisilo na mwisho” ni mfano wa dunia katika machafuko na giza. Kutazamia siku kubwa ya Mungu, Yeremia anatangaza; “Niliangalia inchi, na tazama, ilikuwa ukiwa, haina watu; niliangalia mbingu, nazo hazikuwa na nuru. Niliangalia milima, na tazama, zilitetemeka, na vilima vyote vilitikisika polepole. Nikaangalia, na tazama, hakuna mtu hata mmoja, na ndege zote za mbingu wamekimbia. Nikaangalia, na tazama, shamba lililozaa sana limekuwa jangwa, na miji yake yote ilikuwa imebomoka”. Yeremia 4:23-26.TSHM 320.4

    Hapa ndipo makao ya Shetani pamoja na malaika wake waovu kwa miaka 1000. Amefungiwa kwa dunia hii, hatakuwa na ruhusa ya kuingia kwa dunia zingine kwakujaribu na kusumbua wale ambao hawajaanguka kamwe. Kwa nia hii “amefungwa”. Hakuna anayebakia ambaye anaweza kutumia uwezo wake juu yake. Amekata kwa kazi ya mudanganyifu na uharibifu ambayo ilikuwa anasa yake ya pekee.TSHM 320.5

    Isaya alipokuwa akitazamia maangamizi ya Shetani, anapaza sauti: “Umeanguka toka mbinguni, namna gani, Ee, Lusifero, mwana wa asubui! Umekatwa hata kufika udongo, Wewe uliyeangusha mataifa! Nawe ulisema moyoni mwako: Nitapanda mbinguni, nitanyanyua kiti changu cha enzi juu kuliko nyota za Mungu: ... Nitafanana na Mkuu Sana. Kwani hivi utashushwa mpaka Hadeze, Kwa pande za mwisho za shimo. Wao wanaokuona watakutazama kwa kubanua sana; watakufikiria, wakisema: Huyu ndiye mtu aliyetetemesha dunia, aliyetikisa wafalme; aliyefanya dunia kama jangwa, na aliyeharibu miji yake; yule asiyefungua nyumba ya wafungwa wake? Isaya 14:12-17.TSHM 321.1

    Kwa mda wa miaka 6000, nyumba ya gereza ya Shetani imepokea watu wa Mungu, lakini Kristo amevunja vifungo vyake na kufungua wafungwa. Peke yake pamoja na malaika wake waovu anafahamu moyoni tokeo la zambi: “Wafalme wote wa mataifa, wao wote wanalala katika utukufu, Kila mmoja ndani ya nyumba yake mwenyewe (kaburi);TSHM 321.2

    Lakini wewe umetupwa inje kutoka kaburi lako, Kama tawi linalochukiza... Hutaungwa pamoja nao katika maziko: Kwa sababu umeiharibu inchi yako, na kuua watu wako.” Isaya 14:18-20.TSHM 321.3

    Kwa mda wa miaka 1000, Shetani ataona matokeo ya uasi wake juu ya sheria ya Mungu. Maumivu yake ni mingi sana. Sasa ameachwa kwa kufikiri sana sehemu aliyofanya tangu alipoasi na kutazamia mbele kwa hofu kubwa kwa wakati ujao wa kutisha wakati atakapopashwa kuazibiwa.TSHM 321.4

    Kwa mda wa miaka 1000 katikati ya ufufuo wa kwanza na wa pili, hukumu ya waovu itafanyika. Paulo anaonyesha kwa hii kama tukio linalofuata kurudi kwa Yesu. 1 Wakorinto 4:5. Wenye haki wanatawala kama wafalme na makuhani. Yoane anasema: “Nikaona viti vya enzi, nao wakakaa juu yao vilevile, nao wakapewa hukumu... Watakuwa makuhani wa Mungu na wa Kristo, nao watatawala pamoja naye miaka elfu”. Ufunuo 20:4-6.TSHM 321.5

    Kwa wakati huu “watakatifu watahukumu dunia”. 1 Wakorinto 6:2. Kwa umoja na Kristo wanahukumu waovu, kukata kila jambo kufuatana na matendo yaliyotendwa katika mwili. Ndipo sehemu ambayo waovu wanapaswa kuteswa nayo imetolewa, kufuatana na matendo yao, na imeandikwa juu ya majina yao katika kitabu cha mauti.TSHM 321.6

    Shetani na malaika waovu wamehukumiwa na Kristo na watu wake. Paulo anasema: “Hamujui ya kwamba tutawahukumu malaika”? 1 Wakorinto 6:3. Yuda anatangaza: “Hata malaika wasiolinda enzi yao giza kwa hukumu ya siku ile kubwa”. Yuda 6.TSHM 322.1

    Kwa mwisho wa miaka 1000, ufufuo wa pili utafanyika. Halafu waovu watafufuliwa kutoka katika wafu na kuonekana mbele ya Mungu kwa ajili ya utimilizo wa “hukumu iliyoandikwa”. Zaburi 149:9. Ndivyo Mfunuaji anasema: “Na wafu waliobaki hawakuwa hai hata itimie ile miaka elfu”. Ufunuo 20:5. Na Isaya anatangaza juu ya wenye zambi: “Nao watakusanywa pamoja, kama vile kukusanya kwa wafungwa katika shimo, na watafungwa katika kifungo, na nyuma ya siku nyingi wataangaliwa”. Isaya 24:22.TSHM 322.2

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents