Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents
Tangu Sasa Hata Milele - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    Uzinzi wa Kiroho

    Kanisa, Kutokuwa na uaminifu kwa Kristo katika kuruhusu mambo ya kidunia kutawala moyo ni kama kuvunja kwa kiapo ya ndoa. Zambi ya Israeli katika kumwacha Bwana inaonyeshwa chini ya mfano huu. “Kama vile mke anavyoacha mme wake kwa udanganyifu, ndivyo mulivyonitendea mimi kwa udanganyifu, Ee nyumba ya Israeli, anasema Bwana.” “Mke wa kufanya uasherati! anayekaribisha wageni pahali pa mme wake!” Yeremia 3:20; Ezekieli 16:32.TSHM 183.2

    Asema mtume Yakobo: “Ninyi wazini, hamujui ya kwamba kuwa rafiki ya dunia ni kuwa adui ya Mungu? Basi kila mtu anayetaka kuwa rafiki ya dunia anageuka kuwa adui ya Mungu.” Yakobo 4:4.TSHM 183.3

    Mwanamke (Babeli) yule “amevikwa nguo ya rangi ya zambarau na nyekundu, amepambwa kwa zahabu, na mawe ya bei kubwa, na lulu, naye alikuwa na kikombe cha zahabu mkononi mwake, kinachojaa machukizo, na machafu... Na katika kipaji cha uso wake jina limeandikwa, SIRI, BABELI MKUBWA, MAMA YA MAKAHABA.” Anasema nabii: “Nikaona yule mwanamke amelewa kwa damu ya watakatifu na kwa damu ya washuhuda wa Yesu.” Babeli “ni mji ule mkubwa unaotawala juu ya wafalme wa dunia.” Ufunuo 17:4-6, 18.TSHM 183.4

    Mamlaka ambayo kwa karne nyingi ilidumisha uwezo juu ya wafalme wa jamii ya Wakristo wote ni Roma. Rangi ya zambarau, na nyekundu, zahabu, mawe ya bei kubwa, na lulu, vinaonyesha fahari iliyovaliwa na askofu mwenye kiburi wa Roma. Hakuna mamlaka ingine iliyoweza kutangazwa kwa kweli “amelewa kwa damu ya watakatifu” kama kanisa lile ambalo lilitesa kwa ukali wafuasi wa Kristo.TSHM 183.5

    Babeli inasitakiwa vilevile kwa uhusiano usio wa sheria pamoja na “wafalme wa ulimwengu.” Kwa kuachana na Bwana kupatana na wapagani kanisa la Wayahudi likawa kahaba, na Roma, katika kutafuta usaada wa mamlaka ya kidunia, inapokea hukumu ya namna moja.TSHM 184.1

    “Babeli ni mama ya makahaba.” Binti zake wanapashwa kuwa makanisa yanayoshika mafundisho yake na kufuata mfano wake wa kuacha kweli ili kufanya mapatano pamoja na dunia. Ujumbe unaotangaza kuanguka kwa Babeli unapaswa kulinganishwa na makundi ya ushirika wa dini yaliyokuwa safi zamani na imegeuka kuwa potovu. Kwa hivi ujumbe huu unafuata onyo la hukumu, unapaswa kutolewa katika siku za mwisho. Kwa hiyo haiwezi kutumiwa kwa kanisa la Roma tu, kwa maana lile lilikuwa katika hali ya maanguko muda wa karne nyingi.TSHM 184.2

    Tena, watu wa Mungu wanaitwa kutoka katika Bebeli. Kufuatana na maandiko haya, watu wa Mungu wengi wakingali katika Babeli, Na ni katika makundi gani ya dini ambamo munakuwa sehemu kubwa ya wafuasi wa Kristo? Katika makanisa inayokiri imani ya Kiprotestanti. Kwa wakati wa kutokea kwao makanisa haya yalipata msimamo bora kwa ajili ya kweli, na mibaraka ya Mungu ilikuwa pamoja nao. Lakini wakashindwa kwa tamaa ya namna moja ileile ambayo ilikuwa uharibifu wa Israeli kuiga desturi na kujipendekeza na urafiki wa wasiomwogopa Mungu.TSHM 184.3

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents