Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents
Tangu Sasa Hata Milele - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    Habari llipingwa

    Tangazo la wakati kamili wa kuja kwa Kristo kukaleta mabishano sana kwa wengi wa makundi yote, tokea kwa wachungaji katika mimbara hata kwa mkubwa miongoni mwa wenye zambi. Wengi walitangaza kwamba hawakuwa na kizuizi kwa mafundisho ya kurudi kwa Yesu; walikataa tu wakati kamili. Lakini jicho la Mungu linaloona vyote likasoma mioyo yao. Hawakutamani kusikia habari ya kuja kwa Kristo ili aihukumu dunia kwa haki. Matendo yao hayangevumilia uchunguzi wa moyo unaomtafuta Mungu, na waliogopa kukutana na Bwana wao. Kama Mayahudi kwa wakati wa kuja kwa Kristo kwa mara ya kwanza hawakujitayarisha kumpokea Yesu. Hawakukataa tu kusikiliza mabishano ya wazi kutoka kwa Biblia lakini wakachekelea wale waliokuwa wakitazamia Bwana. Shetani akatupa laumu kwa uso wa Kristo kwamba wanaojidai kuwa watu wake walikuwa na upendo mdogo sana kwake hata hawakutaka kuonekana kwake.TSHM 177.4

    “Hakuna mtu anayejua habari za siku ile na saa ile,” ilikuwa ubishi mara kwa mara ulioendelea kuletwa na waliokataa imani ya kurudi kwa Yesu. Andiko ni: ‘’Habari za siku ile na saa ile hakuna mtu anayejua, hata malaika walio mbinguni, ... ila Baba peke yake.” Matayo 24:36. Maelezo wazi ya maneno haya yalitolewa na wale waliokuwa wakitazamia Bwana, na matumizi mabaya yake ya wapinzani wao yalionyeshwa kwa wazi.TSHM 178.1

    Usemi moja la Mwokozi haupashwi kutumiwa kwa kuharibu lingine. Ingawa hakuna mtu anayejua siku wala saa ya kuja kwake, tunaagizwa kujua wakati unakuwa karibu. Kukataa wala kutojali kujua wakati wa kuja kwake kunapokuwa karibu kutakuwa kwetu kama hatari kwetu kama ilivyokuwa katika siku za Noa bila kujua wakati gani garika ilipashwa kuja. Kristo anasema, “Lakini, usipoangalia, nitakuja kwako kama mwizi, wala hutajua saa nitakapokuja kwako.” Ufunuo 3:3.TSHM 178.2

    Paulo anasema kwa habari za wale waliojali onyo la Mwokozi: “Lakini ninyi ndugu, si katika giza, hata siku ile iwapate ninyi kama mwizi: sababu ninyi wote ni wana wa nuru, na wana wa mchana.” 1 Watesalonika 5:2-5.TSHM 178.3

    Lakini wale waliotamani sababu ya kukataa kweli wakafunga masikio yao kwa maelezo haya, na maneno “Hakuna mtu anayejua siku ao saa” yakaendelea kukaririwa na watu wa zarau na hata wanaojidai kuwa wahubiri wa Kristo. Wakati watu walipoanza kuuliza njia ya wokovu, walimu wa dini wakajitia kati yao na ukweli kwa kufasiri kwa uongo Neno la Mungu.TSHM 178.4

    Waaminifu zaidi katika makanisa walikuwa kwa kawaida wa kwanza kupokea habari. Mahali ambapo watu hawakuwa wakiongozwa na wapadri, mahali ambapo wangeweza kutafuta Neno la Mungu wao wenyewe, mafundisho ya kurudi yalihitaji tu kulinganishwa pamoja na Maandiko juu ya kuimarisha mamlaka yake ya kimungu.TSHM 178.5

    Wengi waliongozwa vibaya na waume, wake, wazazi, ao watoto na walifanywa kuamini jambo hili kama zambi hata kwa kusikiliza mambo ya “uzushi”ya namna hiyo kama iliyofundishwa na Waadventisti. Malaika waliagiza kuwa na ulinzi aminifu juu ya roho hizi, kwa maana nuru ingine ilipaswa kuangaza juu yao kutoka kwa kiti cha Mungu.TSHM 179.1

    Wale waliokubali habari walingojea kuja kwa Mwokozi wao. Wakati ambao walitazamia kukutana naye ulikuwa karibu. Wakakaribisha saa hii kwa utulivu wa heshima. Hakuna aliyekuwa na maarifa hii anayeweza kusahau saa hizo za tamani za kungoja. Kwa maana juma chache mbele ya wakati ule, kazi ya kidunia kwa sehemu kubwa iliwekwa pembeni. Waaminifu wa kweli kwa uangalifu wakachunguza mioyo yao kama kwamba katika saa chache kufunga macho yao kwa maono ya kidunia. Hapo hapakuwa kushona “mavazi ya kupanda nayo” (Tazama Nyongezo), lakini wote wakasikia haja ya ushuhuda wenyewe kwamba walikuwa wakijitayarisha kuonana na Mwokozi. Mavazi yao meupe yalikuwa usafi wa roho--tabia zilizotakaswa na damu ya kafara ya Kristo. Hebu kwamba kungekuwa vivyo na watu wa Mungu na moyo wa namna moja wa kuchunguza, imani yenye juhudi.TSHM 179.2

    Mungu alitaka kuonyesha watu wake. Mkono wake ulifunika kosa katika kuhesabu nyakati za unabii. Wakati wa kutazamia ule ukapita, na Kristo hakuonekana. Wale waliotazamia Mwokozi wao wakajua uchungu mkali. Lakini Mungu alikuwa akichunguza mioyo ya wale waliojidai kungoja kuonekana kwake. Wengi waliongozwa kwa hofu. Watu hawa wakatangaza kwamba hawakuamini kamwe kwamba Kristo atakuja. Walikuwa miongoni mwa wa kwanza kuchekelea huzuni ya waamini wa kweli.TSHM 179.3

    Lakini Yesu na jeshi lote la mbinguni walitazamia kwa upendo na huruma juu ya waaminifu ijapo walikuwa wenye kukatishwa tamaa. Kama kifuniko kinachotenga dunia na vile vinavyoonekana kwa visivyoonekana kikiinuliwa, malaika wangaliweza kuonekana wakisogea karibu na roho hizi za uaminifu na kuzilinda kwa mishale ya Shetani.TSHM 179.4

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents