Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents
Tangu Sasa Hata Milele - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    Mnyama na Sanamu Yake

    Mnyama aliyekuwa na pembe mbili “naye anawafanya wote, wadogo na wakubwa, na matajiri na masikini na wahuru na wafungwa, watiwe chapa katika mkono wao wa kuume, ao katika vipaji vya nyuso zao; na kwamba mtu asiweze kununua wala kuuza asipokuwa na chapa ile, ao jina la mnyama yule, ao hesabu ya jina lake.” Ufunuo 13:16,17. Malaika wa tatu anaonya: “Mtu akiabudu mnyama na sanamu yake, na kupokea chapa katika kipaji cha uso wake, ao katika mkono wake, yeye atakunywa mvinyo ya gazabu ya Mungu.” TSHM 215.2

    “Mnyama” wa hiyo ibada inayolazimishwa ni wa kwanza, ao ya mfano wa chui, nyama wa Ufunuo 13--Kanisa la Roma (Papa). “Sanamu kwa mnyama” ni mfano wa namna ile ya Dini ya Kiprotestanti iliyokufuru ambayo itasitawi wakati makanisa ya Waprotestanti yanapotafuta msaada wa mamlaka ya serkali kwa ajili ya mkazo wa mafundisho ya kanuni zao. “Chapa ya nyama” inaendelea kuelezwa.TSHM 215.3

    Wale wanaoshika amri za Mungu wanakuwa tofauti na wale wanaoabudu mnyama na sanamu yake na kupokea chapa yake. Uchungaji wa sheria ya Mungu, kwa upande moja, na mvunjo wake, kwa upande mwengine, utafanya tofauti kati ya waabudu wa Mungu na waabudu wa mnyama.TSHM 215.4

    Tabia ya kipekee ya mnyama na ya sanamu yake ni kuvunja amri za Mungu. Asema Danieli, juu ya pembe ndogo, kanisa la Roma (Papa): “Atafikiri kugeuza nyakati na sheria.” Danieli 7:25.R.V. Paulo akataja mamlaka ya namna moja “mtu yule wa kuasi” (2 Watesalonika 2:3), aliyejiinua mwenyewe juu ya Mungu. Ila tu kwa kugeuza sheria ya Mungu kanisa la Roma (Papa) liliweza kujiinua lenyewe juu ya Mungu. Mtu ye yote ambaye angeshika sheria kwa kufahamu kama ilivyogeuzwa angekuwa anatoa heshima kubwa kwa sheria za Papa, chapa cha utii kwa Papa pahali pa Mungu.TSHM 215.5

    Kanisa la Roma (Papa) limejaribu kugeuza sheria ya Mungu. Amri ya ine imebadilika hivi kama kuruhusu kushika siku ya kwanza badala ya siku ya saba kama Sabato. Badiliko la kusudi, la kufikiri linaonyeshwa: “Atafikiri kugeuza nyakati na sheria.” Badiliko katika amri ya ine kabisa linatimiza unabii. Hapa uwezo wa Papa unajiweka mwenyewe kwa wazi juu ya Mungu. Waabudu wa Mungu watatofautika kwa kipekee kwa kushika kwao kwa amri ya ine, alama ya uwezo wake wa kuumba. Waabudu wa mnyama watatofautika kwa kufanya nguvu ili kupasua ukumbusho wa Muumba, kuinua sheria ya Roma. Ilikuwa kwa ajili ya Jumapili (siku ya kwanza) kama “siku ya Bwana” ambayo mafundisho ya kanisa la Roma yalitetea kwa mara ya kwanza madai yake ya kiburi. (Tazama Mwisho wa kitabu, Nyongezo). Lakini Biblia inaonyesha siku ya saba kuwa siku ya Bwana. Akasema Kristo: “Basi, Mwana wa watu ndiye Bwana wa sabato vilevile.” Marko 2:28. Utazame tena Isaya 58:13; Matayo 5:1719. Maneno yanayotangazwa mara kwa mara kwamba Kristo aligeuza Sabato yamekataliwa na maneno yake mwenyewe.TSHM 216.1

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents