Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents
Tangu Sasa Hata Milele - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    Froment Mwalimu

    Froment akaanza kazi yake kama mwalimu. Kweli alizofundisha watoto chuoni wakayakariri nyumbani mwao. Mara wazazi wakasikia Biblia ilipokuwa ikielezwa. Agano Jipya na vitabu vidogo vikatolewa bure. Baada ya mda mtumikaji huyu pia alipashwa kukimbia, lakini kweli alizofundisha ikaingia mioyoni mwa watu. Matengenezo yakapandwa. Wahubiri wakarudi, na ibada ya Kiprotestanti ikaanzishwa katika Geneve.TSHM 107.3

    Miji ulikuwa ukmekwisha kutangazwa kuwa upande wa Matengenezo wakati Calvin, alipoingia katika milango yake. Alikuwa njiani kwenda Basel alipolazimishwa kupitia njia ya kuzunguka zunguka kupitia Geneve.TSHM 107.4

    Katika kuzuru huku Farel akatambua mkono wa Mungu. Ingawa Geneve ilikubali imani ya Matengenezo, lakini kazi ya kuongoka ilipaswa kutendeka ndani ya moyo kwa uwezo wa Roho Mtakatifu, si kwa amri za mabaraza. Wakati watu wa Geneve walipokataa mamlaka ya Roma, hawakuwa tayari kabisa kuacha makosa yaliyositawishwa chini ya amri yake.TSHM 107.5

    Kwa jina la Mungu Farel akamsihi kwa heshima mhubiri kijana kudumu na kufanya kazi huko Calvin akarudi nyuma kuonyesha hatari. Akajitenga ili asipambane kwa ha tari na roho ya ukali ya watu wa Geneve. Alihitaji kupata mahali pa amani na ukimya kwa majifunzo, na pale kwa njia ya vitabu angeweza kufundisha na kujenga makanisa. Lakini hakujaribu kukataa. Ilionekana kwake “kwamba mkono wa Mungu ulishuka kutoka mbinguni, kwamba ukamushika, na ukamukaza bila kubadilika kubakia mahali alipokuwa na haraka ya kutoka.”TSHM 107.6

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents