Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents
Tangu Sasa Hata Milele - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    15 / UTAWALA WA KUTISHA WA UFARANSA

    Sababu yake ya Kweli

    Mataifa mengine yalikaribisha Matengenezo kuwa ujumbe wa mbinguni. Katika inchi zingine nuru ya maarifa ya Biblia ilikuwa karibu kufungwa kabisa. Katika inchi ingine kweli na uongo vikashindaniya uwezo kwa karne nyingi. Mwishowe ukweli wa mbinguni ukasongwa. Kiasi cha Roho ya Mungu kikaondolewa kwa watu wale waliozarau zawadi ya neema yake. Na ulimwengu wote ukaona matunda ya kukataa nuru kwa makusudi.TSHM 124.1

    Vita ya kupinga Biblia katika Ufransa ikatimilika wakati wa mapinduzi, ambayo ni matokeo halali kwa Roma kutosoma Maandiko. (Tazama Nyongezo.) Ni onyesho la ajabu sana lililoshuhudia mwisho wa mafundisho ya kanisa la Roma.TSHM 124.2

    Ufunuo ulitangaza matokeo ya kutisha yaliyopaswa kuongezeka zaidi kwa Ufransa kutoka kwa utawala wa “mtu wa zambi”:TSHM 124.3

    “Na kiwanja kilicho inje ya hekalu la Mungu, uache inje, wala usipime kwa maana imetolewa kwa mataifa, nao watakanyaga mji mutakatifu miezi makumi ine na miwili. Nami nitawapa washuhuda wangu wawili nguvu, nao watatoa unabii siku elfu moja mia mbili makumi sita, wamevikwa mavazi ya gunia. ... Hata watakapomaliza ushuhuda wao, yule nyama anayetoka katika shimo pasipo mwisho atafanya vita nao; naye atawashinda na kuwaua. Na maiti yao yatalala katika njia ya mji ule mkubwa, unaoitwa kwa kiroho Sodomo na Misri, ambapo tena Bwana wetu aliposulubiwa. ... Na wale wanaokaa juu ya dunia watafurahi juu yao na kuchekelea, watapelekeana zawadi wao kwa wao, kwa sababu manabii hawa wawili waliwatesa wao wanaokaa juu ya dunia. Na kiisha siku tatu na nusu, Roho ya uhai inayotoka kwa Mungu ikaingia ndani yao, wakasimama kwa miguu yao; na woga mkubwa ukawaangukia watu wote waliowaona.” Ufunuo 11:2-11.TSHM 124.4

    “Miezi makumi ine na miwili” na siku elfu moja mia mbili na makumi sita” ni sawa sawa, wakati ambao kanisa la Kristo lilipaswa kuteswa na magandamizo ya Roma. Miaka 1260 ilianza katika mwaka 538 A.D. na ikamalizika kwa mwaka 1798 AD. (Tazama Nyongezo.) Kwa wakati ule majeshi ya Ufaransa likamfanya Papa kuwa mfungwa, na akafa mbali na kwao. Mamlaka ya Papa ikakosa uwezo wa kuimarisha utawala wake wa zamani.TSHM 124.5

    Mateso hayakudumu hata mwisho katika miaka 1260 yote. Katika huruma zake kwa watu wake, Mungu akafupisha mda wa taabu yao kali kwa mvuto wa Matengenezo.TSHM 125.1

    “Washahidi wawili” ni mfano wa Maandiko ya Agano la Kale na Agano Jipya, washuhuda wakuu kwa mwanzo na umilele wa sheria za Mungu, na pia kwa mpango wa wokovu.TSHM 125.2

    “Nao watatoa unabii siku elfu moja mia mbili makumi sita, wamevikwa mavazi ya gunia.” Wakati Biblia ilipokatazwa, ushuhuda wake ukageuzwa vibaya; wakati wale walipojaribu kutangaza ukweli wake wakasalitiwa, kuteswa, kuuawa kama wafia dini kwa ajili ya imani yao ao kulazimishwa kukimbia--ndipo “washuhuda” waaminifu wakatabiri “katika mavazi ya gunia.” Katika nyakati za giza kabisa watu waaminifu wakapewa hekima na mamlaka kwa kutangaza kweli wa Mungu. (Tazama Nyongezo.)TSHM 125.3

    “Na kama mtu yeyote akitaka kuwaumiza, moto utatoka katika vinywa vyao na kumeza adui zao. Na kama mtu yeyote akitaka kuwaumiza, anapashwa kuuawa namna hii.” Ufunuo 11:5. Watu hawawezi bila kuwa na hofu ya kupata malipizi kwa kuzarau Neno la Mungu!TSHM 125.4

    “Hata watakapomaliza ushuhuda wao.” Wakati washuhuda hawa wawili walipokaribia mwisho wa kazi yao katika giza, vita ilipaswa kufanywa juu yao na “yule nyama anayetoka katika shimo pasipo mwisho.” Hapa kunaonekana onyesho mpya la uwezo wa Shetani.TSHM 125.5

    Ilikuwa busara ya Roma, kushuhudia heshima kwa ajili ya Biblia, kwa kuifungisha kwa lugha isiyojulikana, ikafichwa kwa watu. Chini ya amri yake washahidi wakatabiri “katika mavazi ya gunia. ” Lakini ” yule nyama anayetoka katika shimo pasipo mwisho” alipashwa kufunguliwa na kufanya vita wazi wazi kwa Neno la Mungu.TSHM 125.6

    “Mji mkubwa” katika njia zake ambazo washahidi hawa wawili waliuawa, na mahali maiti yao ililala ni “kwa kiroho” ni Misri. Kwa mataifa yote katika historia ya Biblia, Misri ndiyo iliyozidi kukana kuwako kwa Mungu na ikapinga amri zake. Hakuna mfalme aliyeasi kwa ujasiri sana juu ya mamlaka ya mbingu kama mfalme wa Misri alivyofanya, Farao: “Simjui Bwana, na vilevile sitaruhusu Israeli kwenda.” Kutoka 5:2. Hii ni kusema hakuna Mungu (atheisme), na taifa linalowakilisha Misri lingetaja mfano wa namna moja wa Mungu na kuonyesha roho ya namna moja ya uasi.TSHM 125.7

    “Mji mkubwa” unafananishwa vile vile, “kwa kiroho,” na Sodomo. Maovu ya Sodomo yalionekana zaidi katika uasherati. Zambi hizi zilipaswa kuwa vile vile tabia ya taifa lililopasa kutimiza andiko hili.TSHM 125.8

    Kwa kupatana na nabii, ndipo, mbele kidogo ya mwaka 1798 uwezo moja wa tabia ya uovu ukainuka kwa kufanya vita na Biblia. Na katika inchi ambapo “washuhuda wawili wa Mungu walipashwa kunyamazishwa, hapo pangekuwa onyesho la kutokujali kuwako kwa Mungu kwa Farao na usherati wa Sodomo.TSHM 126.1

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents