Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents
Tangu Sasa Hata Milele - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    Kuvumbua Oroza ya Wakati wa Unabii

    Miller akaendelea na uchunguzi wa mambo ya unabii, wakati wa usiku wote pamoja na wakati wa mchana zikatolewa kwa majifunzo ambayo sasa yalionekana kuwa ya maana kubwa. Katika sura yanane ya Danieli hakuweza kupata dalili kwa mahali halisi pa kuanzia siku 2300; malaika Gabrieli, ingawa aliagizwa kwa kufahamisha Danieli njozi, akamupa tu sehemu ya maelezo. Kwa sababu mateso ya kutisha ilifaa kuanguka juu ya kanisa ilikuwa haikufunuliwa kwa njozi ya nabii, hakuweza kuvumilia tena. Danieli “akazimia, na kugonjwa siku chache.” “Nikashangaa kwa maono,” akasema, “lakini hakuna aliyeyafahamu.” Danieli 8:27.TSHM 154.4

    Lakini Mungu akaagiza mjumbe wake, “Fahamisha mtu huyu maono.” Kwa kutii, malaika akarudi kwa Danieli, kusema: “Nimekuja sasa ili nikupe akili upate kufahamu ... kwa sababu hii elewa maneno haya na kufahamu maono.” Jambo moja la maana katika sura ya 8 liliachwa bila kufasiriwa, yaani, siku 2300; kwa hiyo malaika, kwa kuendelea na maelezo yake, akaeleza sana juu ya wakati:TSHM 154.5

    “Mda wa majuma makumi saba umeamriwa juu ya watu wako na juu ya mji wako mtakatifu... Ujue basi na kufahamu ya kuwa tangu kuwekwa amri ya kutengeneza na kujenga Yerusalema hata mupakaliwa, masiya mkubwa, yatakuwa majuma saba na majuma makumi sita na mawili; njia kuu itajengwa tena, na ukuta, hata katika nyakati za taabu. Na nyuma ya majuma makumi sita na majuma mawili massiah atakataliwa mbali, lakini ni kwake mwenyewe: ... Naye atafanya agano la nguvu pamoja na wengi kwa juma moja: na kwa nusu ya juma atakomesha kafara na toleo.” Danieli 8:16; 9:22,23, 24-27.TSHM 155.1

    Malaika alitumwa kwa Danieli kwa kueleza jambo aliloshindwa kufahamu “Hata mangaribi na asubui ya siku elfu mbili mia tatu; ndipo Pahali patakatifu patasafishwa.” Maneno ya kwanza ya malaika ni haya, “Mda wa majuma makumi saba umeamriwa juu ya watu wako na juu ya mji wako.” Neno umeamriwa kwa halisi maana yake “atakatiliwa mbali.” Majuma makumi saba, miaka 490, ilipaswa kukatiliwa mbali kuwekwa kando kwa ajili ya Wayahudi.TSHM 155.2

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents