Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents
Tangu Sasa Hata Milele - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    Ujumbe wa Wanafunzi Ulilinganishwa na Ujumbe wa 1844

    Maarifa ya wanafunzi kwa kuja kwa mara ya kwanza kwa Kristo yalikuwa na sehemu yake katika maarifa ya wale waliotangaza kuja kwake kwa mara ya pili. Kama vile wanafunzi walivyohubiri, “Wakati umetimia, ufalme wa Mungu ni karibu,’‘ vilevile Miller na washiriki wake walitangaza kwamba mda wa unabii wa mwisho katika Biblia ulikuwa karibu kuisha, kwamba hukumu ilikuwa karibu, na kwamba ufalme wa milele ulipashwa kuingizwa. Mahubiri ya wanafunzi kwa habari ya nyakati yalisimamia juu ya majuma makumi saba ya Danieli 9. Ujumbe uliotolewa na Miller na washiriki wake ulitangaza mwisho wa siku 2300 za Danieli 8:14, mahali ambamo majuma makumi saba yanakuwa Sehemu moja. Mahubiri ya kila mojawapo yalisimamia juu ya utimilifu wa sehemu mbalimbali za mda wa unabii ule ule.TSHM 167.2

    Kama wanafunzi wa kwanza, William Miller na washiriki wake hawakufahamu kabisa ujumbe waliuochukua. Makosa yaliyoanzishwa mda mrefu katika kanisa yakazuia maelezo sahihi ya jambo kubwa katika unabii. Kwa hiyo, ijapo walitangaza ujumbe ambao Mungu aliwatolea, lakini katika kukosa kufahamu maana yake wakateseka kwa kukata tamaa.TSHM 167.3

    Miller akaingiza maoni ya kawaida kwamba dunia ni “mahali patakatifu,” na akaamini kwamba “kutakasika kwa mahali patakatifu” kulionyesha kutakasika kwa dunia na moto kwa kuja kwa Bwana. Kwa hiyo, mwisho wa siku 2300, akazani, zilifunua wakati wa kuja kwa Yesu mara ya pili.TSHM 167.4

    Kutakaswa kwa mahali patakatifu ilikuwa kazi ya mwisho iliyofanywa na kuhani mkuu katika utaratibu wa huduma wa mwaka. Ilikuwa ni kufunga kazi ya upatanisho--kuondoa ao kuweka mbali zambi za Israeli. Ilionyesha picha la kufunga kazi ya Kuhani Mkuu wetu mbinguni katika kuondoa ao kufutia mbali zambi za watu wake zilizoandikwa katika vitabu mbinguni. Kazi hii inaleta uchunguzi, kazi ya hukumu, na inatangulia bila kukawia kuja kwa Kristo katika mawingu ya mbingu, kwani atakapokuja kila jambo litakuwa limekwisha kukatwa. Asema Yesu: “Na mshahara wangu ni pamoja nami, kulipa kila mtu kama ilivyo kazi yake.” Ufunuo 22:12. Ni hii kazi ya hukumu inayotangazwa na ujumbe wa malaika wa kwanza wa Ufunuo 14:7. “Ogopeni Mungu, na kumutukuza kwa maana saa ya hukumu yake imekuja.”TSHM 168.1

    Wale waliotangaza onyo hili walitoa ujumbe wa haki kwa wakati unaofaa. Namna wanafunzi walikuwa hawakufahamu juu ya ufalme wa kusimamishwa kwa mwisho wa “majuma makumi saba,” vivyo hivyo Waadventisti hawakufahamu habari ya jambo lililopashwa kufanyika kwa mwisho wa “siku 2300.” Katika mambo mawili haya makosa inayopendwa na watu wengi ikapofusha akili kwa kutojua ukweli. Wote wawili wakatimiza mapenzi ya Mungu kwa kutoa ujumbe aliotamani utolewe, na wote wawili katika kukosa kufahamu maana ya ujumbe wao wakateseka kwa kukata tamaa.TSHM 168.2

    Lakini Mungu alitimiza kusudi lake katika kuruhusu onyo la hukumu kutolewa kama ilivyokuwa. Katika maongozi yake ujumbe ulikuwa kwa ajili ya uchunguzi na utakaso wa kanisa. Je, upendo wao ulikuwa juu ya dunia ao juu ya Kristo na mbingu? Je walikuwa tayari kuacha tamaa zao mbaya za dunia na kukaribisha kuja kwa Bwana wao?TSHM 168.3

    Uchungu vile ungechunguza mioyo ya wale waliojidai kupokea onyo. Je, wangetupilia mbali tumaini lao katika Neno la Mungu walipoitwa kwa kuvumilia makemeo ya dunia na jaribu la kukawia na kukata tamaa? Kwani hawakufahamu mara moja mambo ya Mungu, je wangetupa pembeni kweli iliyo kubaliwa na ushuhuda wazi wa Neno lake? Jaribu hili linge fundisha hatari ya kukubali maelezo ya watu baadala ya kufanya Biblia mtafsiri wake mwenyewe. Watoto wa imani wangeongozwa kujifunza kwa bidii sana Neno, na kuchunguza kwa uangalifu zaidi msingi wa imani yao, na kukataa kila kitu, hata kilikubaliwa sana na Wakristo wa kidunia, kile kisichokuwa na msingi kutika kwa Maandiko.TSHM 168.4

    Kile ambacho katika saa ya taabu kilionekana giza baadaye kingewekwa wazi. Ijapokuwa taabu ilitokea kwa makosa yao, wangejifunza kwa maarifa ya mibaraka yao kwamba Bwana ni ” Mwenye rehema sana, mwenye huruma”, kwamba njia zote zake ni ” huruma na kweli kwao wanaoshika agano lake na shuhuda wake.” Yakobo 5:11; Zaburi 25:10. ” Hata mangaribi na asubui 2300: halafu Pahali patakatifu patasafishwa.”TSHM 169.1

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents