Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents
Tangu Sasa Hata Milele - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    Pahali Patakatifu na Patakatifu pa Patakatifu

    Katika Pahali patakatifu kulikuwa na kinara upande wa kusini pamoja na taa zake saba kutoa nuru mchana na usiku; upande wa kaskazini kulikuwa na meza ya mikate ya onyesho. Mbele ya pazia inayotenga Pahali patakatifu na patakatifu pa patakatifu kulikuwa na mazabahu ya zahabu ya uvumba, ambalo wingu la manukato, pamoja na maombi ya Israeli, yalikuwa yakipanda kila siku mbele za Mungu.TSHM 197.1

    Katika Pahali patakatifu pa patakatifu palisimama sanduku, sanduku ilifunikwa na zahabu, gala ya Amri Kumi. Juu ya sanduku kulikuwa na kiti cha rehema kilichokuwa na makerubi wawili waliofanywa na zahabu ngumu. Ndani ya chumba hiki kuwako kwa Mungu kulionekana katika wingu utukufu lililokuwa katikati ya kerubi.TSHM 197.2

    Baada ya kuwekwa kwa Waebrania katika Kanana, hema ao maskani iliwakombolewa kwa hekalu ya Solomono, ambayo, ijapo ni ya umbo la daima na ya ukubwa wa juu, ikafuata ulinganifu wa namna moja na vyombo vivyo hivyo. Katika umbo hili hema likawako--isipokuwa kwa wakati wa maangamizi wakati wa Danieli-hata maharibifu yake iliyofanywa na wa Waroma katika mwaka A.D. 70. Hii ni Pahali patakatifu tu duniani ambapo Biblia inatoa maelezo yote, Pahali patakatifu pa agano la kwanza. Lakini agano jipya halina Pahali patakatifu?TSHM 197.3

    Kurudi tena kwa kitabu cha Waebrania, wakatafuta ukweli wakaona kwamba Pahali patakatifu pa agano la pili ao jipya ilionyeshwa katika maneno yaliyokwisha kuelezwa vizuri: “Basi hata agano la kwanza lilikuwa na amri ya kuabudu Mungu, na Pahali patakatifu pake pa dunia.” Kurudi nyuma kwa mwanzo wa sura ya kwanza, wanasoma: “Basi, neno kubwa katika maneno haya tunasoma ni hii: Tuna kuhani mukubwa wa namna hii, aliyeketi mukono wa kuume wa kiti cha Mwenyezi katika mbingu, mutumishi wa Pahali patakatifu, na wa hema ya kweli, ndiyo Bwana aliisimamisha, wala si watu.” Waebrania 8:1,2.TSHM 197.4

    Hapa panafunua Pahali patakatifu pa agano jipya... Pahali patakatifu pa agano la kwanza ilitengenezwa na Musa; hii ilitengenezwa na Bwana. Katika patakatifu pale pa kidunia makuhani walikuwa wakitenda huduma yao; katika hii, Kristo, Kuhani wetu Mkuu, alihudumia kwa mukono wa kuume wa Mungu. Hema takatifu moja ilikuwa duniani, na ingine ilikuwa mbinguni.TSHM 197.5

    Hema iliyojengwa na Musa ilifanywa kwa mfano. Bwana alipokuwa akionyesha: “Sawasawa na maneno yote ninayokuonyesha, mufano wa hema, mfano wa vyombo vyake vyote, ndivyo mutakavyofanya.” “Na angalia uvifanye kwa mufano wao ulioonyeshwa mulimani.” Hema ya kwanza ilikuwa “mufano wa wakati wa sasa; ndani yake sadaka na zabihu zilitolewa”, mahali pake takatifu “mifano ya vitu vilivyo mbinguni.” Makuhani walikuwa wakitumika kwa mufano na kivuli cha vitu vya mbinguni.” Kristo hakuingia katika Pahali patakatifu palipofanywa kwa mikono, ndio mufano wa kweli, lakini aliingia mbinguni zenyewe, aonekane sasa mbele ya Mungu kwa ajili yetu.” Kutoka 25:9,40; Waebrania 9:23; 8:5; 9:24.TSHM 198.1

    Hema ya mbinguni ni asili kubwa ya hema Musa alijenga ambayo ilikuwa ni mfano. Fahari ya hema ya kidunia ilikuwa mfano wa utukufu wa hekalu lile la mbinguni pahali Kristo anapohudumia kwa ajili yetu mbele ya kiti cha ezi cha Mungu. Ukweli wa maana juu ya hema ya mbinguni na ukombozi wa mwanadamu yalifundishwa na Pahali patakatifu pa kidunia na huduma zake.TSHM 198.2

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents