Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents
Tangu Sasa Hata Milele - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    Adui Mwangalifu

    Adui huyu mwangalifu yuko anajiingiza katika kila jamaa, katika kila njia, katika makanisa, katika ma Baraza ya mataifa, katika manyumba ya sheria, katika baraza za hukumu, Kuleta matatizo, kudanganya, kukosesha, po pote kuharibu nafsi na miili ya wanaume na wanawake, na watoto. Anaharibu jamaa, kupanda uchuki, vita, fitina, na uuaji wa mtu kwa kusudi. Na ulimwengu unaonekana kuzania mambo haya kama kwamba ni Mungu aliyeyaweka na yanapashwa kuwako. Wote wasiokusudia kuwa wafuasi wa Kristo wanakuwa watumishi wa Shetani. Wakati Wakristo wanapochagua jamii ya wasiomwogopa Mungu, wanajihatarisha wao wenyewe kwa majaribu. Shetani anajificha mwenyewe kwa macho na anafunika kifuniko chake cha udanganyi kwa macho yao.TSHM 247.1

    Kufuatana na desturi za dunia anageuza kanisa kwa dunia, hageuzi kamwe dunia kwa Kristo. Kujizoeza zambi kutaifanya isionekane kuwa mbaya sana. Wakati katika njia ya kazi tunaletwa katika kujaribiwa, tunaweza kuwa na hakika kwamba Mungu atatulinda; lakini tukijiweka sisi wenyewe chini ya jaribu tutaanguka upesi ao baadaye.TSHM 247.2

    Mjaribu mara kwa mara anatumika kwa mafanikio zaidi katika wale bila shaka wasiojizania kuwa chini ya mamlaka yake. Kipawa na elimu ni kimtu ni zawadi za Mungu; lakini wakati hizi zinapoongoza mbali kutoka kwake, zinakuwa mtego. Mara nyingi mtu mwenye elimu ya akili na wa tabia ya kupendeza ni chombo kizuri katika mikono ya Shetani.TSHM 247.3

    Musisahau kamwe onyo la maongozi ya Mungu la kutangaza tangu karne nyingi hata wakati wetu. “Muwe na kiasi na kuangalia; mpinzanii wenu Shetani, kama simba anayenguruma anayezungukazunguka akitafuta mtu amumeze.” “Vaeni silaha zote za Mungu, mupate kuweza kusimama juu ya hila za Shetani.” 1 Petro 5:8; Waefeso 6:11. Adui wetu mkubwa anajitayarisha kwa mashambulio yake ya mwisho. Wote wanaomfuata Yesu watakuwa katika vita pamoja na adui huyu. Zaidi sana Mkristo anapoiga Mfano wa Mungu, na zaidi hakuna shaka atajiweka mwenyewe alama kwa mashambulio ya Shetani.TSHM 247.4

    Shetani alishambulia Kristo kwa majaribu makali na hila; lakini alikomeshwa katika kila vita. Kushinda kule kote kunatuwezesha sisi kishinda. Kristo atatoa nguvu kwa wale wote wanaoitafuta. Hakuna mtu asipokubali yeye mwenyewe anaweza kushindwa na Shetani. Mjaribu hana uwezo wa kutawala mapenzi ao kulazimisha mtu kufanya zambi. Anaweza kutia ao kuanzisha taabu, lakini hapana uchafu. Jambo la hakika kwamba Kristo alishinda linapasa kutia moyo wafuasi wake kwa nguvu kupigana vita juu ya zambi na Shetani.TSHM 248.1

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents