Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents
Tangu Sasa Hata Milele - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    Kuweka Kando Sheria ya Mungu

    Wale wanaofundisha watu kutunza sheria za Mungu kwa urahisi wanapanda uasi kwa kuvuna uasi. Kuacha amri iliyoamuriwa kwa sheria ya Mungu kuweka yote kando, na sheria za kibinadamu kwa upesi hazitajaliwa. Matokeo ya kutangua amri za Mungu ingekuwa kama hazikutumainiwa. Mali hayangekuwa tena na usalama. Watu wangekamata milki ya jirani zao kwa jeuri, na walio hodari zaidi wangekuwa watajiri kuliko. Maisha yenyewe hayangeheshimiwa Kiapo cha ndoa hakingedumu tena kuwa kama boma kwa kulinda jamaa. Yeye aliyekuwa na uwezo angekamata mke wa jirani yake kwa jeuri. Amri ya tano ingekuwa kando pamoja na ya ine. Watoto hawangekataa kukamata maisha ya wazazi wao kama kwa kufanya vile wangeweza kupata tamaa ya mioyo yao iliyoharibika. Ulimwengu uliostaarabika ungekuwa kundi la wezi na wauaji wa siri, na amani na furaha ingekomeshwa duniani.TSHM 285.1

    Tayari mafundisho haya yamefungua milango ya uovu ulimwenguni. Bila sheria na uovu vinafiagia kama pepo kali ya kipwa. Hata katika nyumba za wale wanaojidai kuwa Wakristo kunakuwa unafiki, mvunjo wa urafiki, usaliti wa matumaini matakatifu, upendeleo wa tamaa mbaya. Kanuni za dini, msingi wa maisha ya ushirika, unaonekana wa kutikisika sana karibu kuanguka. Wavunja sheria waovu mara kwa mara wanafanywa kuwa wenye kupokea mambo ya uangalifu kama kwamba walifikia sifa nzuri. Matangazo makubwa yametolewa kwa makosa yao. Mtambo wa kupiga chapa unatangaza maelezo ya uasi wa uovu, kuingiza wengine katika madanganyo, wizi, na uuaji. Kupumbazuka kwa kosa, kukosa kuwa na kiasi kwa kutisha na uzalimu wa namna yo yote ulipasa kuamsha mambo yote. Ni kitu gani kinaweza kufanyika kuzuia mwendo wa uovu?TSHM 285.2

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents