Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents
Tangu Sasa Hata Milele - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    36 / MAPIGANO YA KARIBU SANA

    Tangu mwanzo kabisa wa vita kubwa mbinguni, kusudi daima la Shetani lilikuwa kuvunja sheria ya Mungu. Kwa yeye kufikia kusudi lake ni kukataa sheria yote ama kukataa mojawapo ya amri zake, matokeo yatakuwa namna moja. Mtu anayekosa “katika neno moja tu” anaonyesha zarau kwa sheria yote; mvuto wake na mfano yanakuwa kwa upande wa kosa; anakuwa mwenye kukosa juu ya yote”. Yakobo 2:10.TSHM 284.1

    Shetani amepotesha mafundisho ya Biblia, na kwa hivi makosa yakaingia katika imani ya maelfu. Mapigano makubwa ya mwisho kati ya ukweli na uwongo ni juu ya amri ya Mungu, kati ya Biblia na dini ya uwongo na mambo ya asili. Biblia inafikia wote, lakini wachache tu wanaoikubali kama kiongozi cha uzima. Katika kanisa wengi wanakana nguzo za imani ya Kristo. Uumbaji, kuanguka kwa mtu, upatanisho wa Yesu Kristo kwa kufa kwake, na sheria ya Mungu hutawaliwa yote ao sehemu. Maelfu wanaizania kuwa kama ushuhuda wa uzaifu kuweka tumaini kamili katika Biblia.TSHM 284.2

    Ni rahisi kufanya sanamu na maelezo ya uwongo kama kufanya sanamu ya mti ao jiwe. Kwa kueleza Mungu vibaya, Shetani anaongoza watu kumzania katika tabia ya uwongo. Sanamu ya utilivu imewekwa katika pahali pa Mungu mwenye uhai kama anavyofuniliwa katika Neno lake, katika Kristo, na katika kazi ya uumbaji. Mungu wa watu hodari wengi, watunga mashairi, watu wa siasa, waandishi wa habari kwa magazetu-wa vyuo vikubwa (universités) vingi, hata wavyama vya elimu ya tabia na za Mungu na dini (théologie) ni afazali kidogo kuliko Bali, mungu wa jua wa Foiniki katika siku za Eliya. Hapana kosa linalofika kwa ujasiri zaidi juu ya mamlaka ya Mungu, hapana linalokuwa mbaya zaidi katika matukio yake, kuliko mafundisho ya kwamba sheria ya Mungu haina na masharti tena. Ufikiri ya kama wahuduma wenye kujulikana walikuwa wakifundisha kwa wazi ya kuwa sheria zinazotawala inchi yao hazikuwa za lazima, ya kama zilizuia mambo ya uhuru wa watu na haiwapashwi kutiiwa; muda gani watu kama wale wangevumiliwa katika mimbara?TSHM 284.3

    Ingekuwa muaminifu zaidi kwa mataifa kuvunja sheria zao kuliko kwa mtawala wa viumbe vyote kutangua sheria yake. Jaribio la kufanya nafasi sheria ya Mungu lilijaribiwa katika Ufransa wakati kukana Mungu ulipokuwa na uwezo wa kutawala. Ilionyeshwa ya kwamba kwa kutupa amri ambazo Mungu aliamuru ni kukubali kanuni ya mtawala wa uovu.TSHM 284.4

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents