Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents
Tangu Sasa Hata Milele - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    Ujumbe Ulitolewa kwa Wakati Uliofaa

    Kwa namna ileile Miller na washiriki wake wakatimiza unabii na wakatoa ujumbe ambao Maongozi ya Mungu yalitabiri ulipashwa kutolewa kwa ulimwengu. Hawangeweza kuutoa wangefahamu kabisa mambo ya unabii yanayoelekea uchungu wao, na kutoa ujumbe mwengine kuhubiriwa kwa mataifa yote kabla ya kuja kwa Bwana. Habari za malaika wa kwanza na wa pili zilitolewa kwa wakati unaofaa na zilitimiza kazi ambayo Mungu aliyokusudia waitende.TSHM 193.3

    Dunia ilikuwa ikitazamia kwamba kama Kristo hangetokea, Kiadventiste kingeachwa . Lakini wakati watu wengi walipoacha imani yao kulikuwa wengine waliosimama imara. Matunda ya kazi ya adventiste, roho ya uchunguzi wa moyo, ya kukana dunia na kutengeneza maisha, ikashuhudia kwamba ilikuwa kazi ya Mungu. Hawakusubutu kukana kwamba Roho Mtakatifu alishuhudia kwa mahubiri ya kuja kwa Yesu mara ya pili. Hawakuweza kuvumbua kosa katika nyakati maalum za unabii. Adui zao hawakufaulu kuangusha maelezo yao ya unabii. Hawakuweza kukubali kukana msimamo uliofikiwa kwa njia na juhudi, kujifunza Maandiko kwa maombi, katika akili zilizoangaziwa na Roho wa Mungu na mioyo ya kuchomwa kwa uwezo wake wenye uzima, ambao ulisimama imara na kupinga watu wa elimu na usemaji.TSHM 193.4

    Waadventiste waliamini kwamba Mungu aliwaongoza kutoa onyo la hukumu. Wakatangaza, “limechunguza mioyo ya wote waliolisikia, ... ili wale watakaochunguza mioyo yao wenyewe, waweze kujua upande gani ... wangepatikana, kama Bwana angefika sasa wangepaza sauti, `Huyu ndiye Mungu wetu, Tumemungoja, naye atatuokoa;’ ao wangeita miamba na milima kuanguka juu yao kuwaficha mbele ya uso wake yeye anayeketi juu ya kiti cha enzi!TSHM 194.1

    Mawazo ya wale walioendelea kuamini kwamba Mungu aliongoza yanaelezwa katika maneno ya William Miller: “Tumaini langu katika kuja kwa Kristo ni la nguvu kwa daima, nimefanya tu, baada ya miaka ya uangalifu, kila nilichoona wajibu wangu kufanya.” “Maelfu mengi, kwa mfano wote wa kibinadamu, walifanywa kwa kujifunza Maandiko katika mahubiri ya wakati; na kwa njia ile, katika imani na kumwangiwa kwa damu ya Kristo, wamepatanishwa kwa Mungu.”TSHM 194.2

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents