Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents
Tangu Sasa Hata Milele - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    37 / MAANDIKO MLINDA SALAMA YETU PEKEE

    Watu wa Mungu wanaongozwa kwa maandiko kama mlinda usalama wao kwa kupinga mvuto wa wa waalimu wa uongo na roho za giza. Shetani hutumia kila shauri lo lote iwezekanavyo kuzuia watu kupokea maarifa ya Biblia, kwa usemi ao maneno yake ya waziinafunua madanganyifu yake. Madanganyo makubwa ya mwisho ni karibu kufunguliwa mbele yetu. Mpinga Kristo atafanya kazi yake ya ajabu mbele ya macho yetu kwa ukaribu kutakuwa mfano wa kufanana na iliyo ya kweli ambayo itakuwa haiwezekani kutofautisha kati yao isipokuwa kwa Maandiko. Wale wanaojitahidi kutii amri zote za Mungu watapingwa na kuzarauliwa. Kwa kuvumilia jaribu, wanapaswa kufahamu mapenzi ya Mungu kama inavyofuniliwa katika Neno lake. Hapana mtu bali wale ambao wamaimarisha akili kwa kweli za Biblia watakaosimama katika vita kubwa ya mwisho.TSHM 290.1

    Mbele ya kusulibiwa kwake mwokozi alielezea wanafunzi wake ya kama alipashwa kuuawa na kufufuka tena. Lakini maneno yaliondolewa mbali kutoka kwa mawazo ya wanafunzi. Wakati jaribu lilipofika, kifo cha Yesu kikaharibu kabisa matumaini yao kama kwamba hakuwaonya mbele. Kwa hivyo katika mambo ya unabii na wakati ujao umefunuliwa wazi mbele yetu kwa kama ulivyofunuliwa kwa wanafunzi na Kristo mwenyewe. Tukio zinazo ambatana na wakati wa kufungwa wakati wa majaribu na kazi ya matayarisho kwa wakati wa taabu yanaonyeshwa wazi. Lakini wengi hawanaufahamu wa kweli hizi za maana sana, na wakati wa taabu utafika utawakuta wasiokuwa tayari.TSHM 290.2

    Wakati Mungu anapotuma maonyo, anaagiza kila mtu kujaliwa na sababu kwa kukubali ujumbe. Hukumu za kutisha juu ya kuabudu mnyama na sanamu yake(Ufunuo 14:9-11) inapashwa kuongoza wote kujifunza namna alama ya mnyama inavyokuwa na namna gani ya kuepuka kuipokea. Lakini jamii ya watu hawataki ukweli wa Biblia, kwa sababu unazuia tamaa za moyo wa zambi. Shetani anatoa mambo ya udanganyifu wanaopenda.TSHM 290.3

    Lakini Mungu atakuwa na watu watakaodumisha Biblia, na ni Biblia peke yake, kama kawaida ya mafundisho yote na msingi wa matengenezo yote. Nia za watu waliojifunza, matoleo ya elimu ya kweli, makusudi ya baraza za kanisa, sauti ya watu wengi-hakuna mojawapo ya haya yanapashwa kuzaniwa kama ushahidi kwa kukubaliana ao kutokubali mafundisho yo yote. Inatupasa kudai zahiri “Bwana anasema hivi”. Shetani anaongoza watu kutazama kwa wachungaji, kwa waalimu wa elimu ya tabia na sifa za Mungu na dini kama viongozi vyao, badala ya kuchunguza Maandiko wao wenyewe. Kwa kutawala waongozi hawa, anaweza kuvuta wengi.TSHM 290.4

    Wakati Kristo alipokuja, watu wa kawaida walimsikia kwa furaha. Lakini mkuu wa ukuhani na watu wenye kuongoza wakajiingiza wao wenyewe katika uzalimu; wakakataa ushuhuda wa Umasiya wake. “Namna gani inakuwa”, watu wakauliza, “ya kama watawala wetu na wandishi waliojifunza hawaamini Yesu? Waalimu kama wale walioongoza taifa la Wayuda kukataa Mkombozi wao.TSHM 291.1

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents