Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents
Tangu Sasa Hata Milele - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    lla tu Kwa Njia ya Imani

    Kazi hii inaweza kutimizwa tu kwa njia ya imani katika Kristo, kwa uwezo wa kukaa ndani ya Roho ya Mungu. Mukristo atajisikia mwenye mivuto ya zambi, lakini atashikilia vita isiyobadilika juu yake. Hapa ndipo msaada wa Kristo unahitajiwa. Uzaifu wa binadamu unaambatana na nguvu za kimungu, na imani inapaza sauti: “Asante kwa Mungu anayetupa sisi ushindi kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo.” 1 Wakorinto 15:57.TSHM 227.3

    Kazi ya utakaso ni ya kuendelea mbele. Wakati katika toba mwenye zambi anapopata amani pamoja na Mungu maisha ya Mukristo imeanza tu. Sasa anapashwa kuendelea katika ukamilifu,” kukua “hata kufika kipimo cha kimo cha wa utimilifu wa Kristo.” “Ninakaza mwendo hata nifikie mwisho wa zawabu ya mwito mukubwa wa Mungu katika Kristo Yesu.” Waebrania 6:1; Waefeso 4:13; Wafilipi 3:14.TSHM 227.4

    Wale wanaozoea maisha ya utakaso wa Biblia wataonyesha unyenyekevu. Wanaona kutostahili kwao wenyewe katika tofauti pamoja na ukamilifu wa Mungu. Nabii Danieli alikuwa mufano wa utakaso wa kweli. Badala ya kujitangaza kuwa safi na mtakatifu, nabii huyu wa heshima akajitambulisha mwenyewe pamoja na wenye zambi wa kweli wa Israeli wakati alipokuwa akimlilia Mungu kwa ajili ya watu wake. Danieli ; 9:15,18,20; 10:8,11.TSHM 227.5

    Hapawezi kuwa kujiinua mwenyewe, hapana madai ya kujisifu kwa uhuru wa zambi kwa upande wa wale wanaotembea katika kivuli cha msalaba wa Kalvari. Waliona kwamba ilikuwa ni zambi yao ambayo ilianzisha maumivu makuu yaliyovunja moyo wa Mwana wa Mungu, na wazo hili litaongoza kwa kujinyenyekeza. Wale wanaoishi karibu sana na Yesu wanatambua wazi zaidi uzaifu na hali ya zambi ya wanadamu, na tumaini lao moja tu linakuwa katika tabia nzuri ya Mwokozi aliyesulibiwa na kufufuka.TSHM 228.1

    Utakaso sasa unaoendelea mbele kwa sifa katika watu wa dini unaeneza roho ya kujiinua na kutojali kwa sheria ya Mungu ambayo inauonyesha kama jambo la kigeni kwa Biblia. Watetezi wake hufundisha kwamba utakaso ni kazi ya dakika moja, ambayo, katika “imani tu,” wanafikia utakatifu kamili. “Uamini tu,” wanavyosema, “na mibaraka ni yako.” Hapana juhudi ya zaidi kwa upande wa mwenye kupokea inayopashwa kufanywa. Kwa wakati ule ule wakakataa mamlaka ya sheria ya Mungu, kushurutisha kwamba wamewekwa huru kwa kanuni ya kushika amri. Lakini inawezekana kuwa mutakatifu pasipo kuja katika umoja na kanuni ambazo zinaonyesha tabia ya Mungu na mapenzi yake?TSHM 228.2

    Ushuhuda wa Neno la Mungu unakuwa kinyume cha mafun-disho haya ya mtego ya imani pasipo matendo. Si imani inayotafuta kibali cha Mungu bila kushika tabia inayohitajiwa kwa ajili ya rehema ya kutolewa. Ni kiburi. Tazama Yakobo 2:14-24.TSHM 228.3

    Hebu watu wasijidanganye wenyewe kwamba wanaweza kuwa watakatifu wanapovunja kwa makusudi mojawapo ya matakwa ya Mungu. Zambi inayojulikana inanyamazisha ushuhuda wa sauti ya Roho na inatenga nafsi toka kwa Mungu. Ingawa Yoane alidumu kabisa juu ya mapendo, hakusita kufunua tabia ya kweli ya kundi linalojidai kuwa takatifu wakati wanapoishi katika kuvunja sheria ya Mungu. “Yeye anayesema; Nimemujua, wala hashiki amri zake, ni mwongo, wala kweli si ndani yake. Lakini yeye anayeshika neno lake, katika huyu mapendo ya Mungu yamekamilishwa kweli kweli.” 1 Yoane 2:4,5. Hapa kuna jaribio ya ushuhuda wa kila mtu. Kama watu wanapungua na kuzarau amri za Mungu, kama “wakivunja amri moja katika hizi zilizo ndogo, na kufundisha watu hivyo” (Matayo 5:18,19), tunaweza kujua kwamba madai yao hayana msingi.TSHM 228.4

    Kusema hana zambi ni ushuhuda kwamba yeye anatangaza haya anakuwa mbali kwa utakatifu. Hana wazo la kweli la usafi usiokuwa na mwisho na utakatifu wa Mungu, na uovu na ubaya wa zambi. Zaidi anajitenga mbali kwa Kristo,zaidi anajiona yeye mwenyewe kuwa mwema.TSHM 228.5

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents