Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents
Tangu Sasa Hata Milele - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    Vyumba Viwili

    Nafasi takatifu za mahali patakatifu mbinguni zinafananishwa na vyumba viwili katika Pahali patakatifu duniani. Yohana alijaliwa na maono ya hekalu ya Mungu mbinguni. Alitazama kule “taa saba za moto ziliwaka mbele ya kiti cha enzi.” Aliona malaika “mwenye chungu cha zahabu ya uvumba; akapewa uvumba mwingi, ili autie pamoja na maombi ya watakatifu wote juu ya mazabahu ya zahabu iliyo mbele ya kiti cha enzi.” Ufunuo 4:5; 8:3. Hapa nabii akaona chumba cha kwanza cha Pahali patakatifu pa mbinguni; na aliona “taa saba za moto” na “mazabahu ya zahabu”, iliyofananishwa kwa kinara cha zahabu na mazabahu ya uvumba katika Pahali patakatifu pa dunia.TSHM 198.3

    Tena ‘’hekalu la Mungu likafunguliwa”, na akatazama ndani ya pazia juu ya patakatifu pa patakatifu. Na akaona “sanduku ya agano lake” la kufananishwa na sanduku lililojengwa na Musa kwa kuweka ndani amri ya Mungu. Ufunuo 11:19.TSHM 198.4

    Hivyo, wale wanaojifunza fundisho hili wakaone bila shaka kwamba hakika mbinguni kunakuwa hema. Musa alijenga hema ya kidunia akifuata mfano alioonyeshwa. Paulo anafundisha kuwa mfano ule ulikuwa hema ya kweli ambao unakuwa mbinguni. Na Yoane anashuhudia kwamba aliiona mbinguni.TSHM 198.5

    Ndani ya hekalu mbinguni, Pahali patakatifu pa patakatifu kunakuwa amri ya Mungu. Sanduku inayowekwa amri inafunikwa na kiti cha rehema, ambapo mbele yake Yesu anatetea mwenye zambi kwa ajili ya damu yake. Hapa ndipo kunafananishwa muungano wa haki na rehema katika mpango wa wokovu, muungano ambao unashangaza mbingu yote mzima. Hii ndiyo siri rehema ambamo malaika wanatamani kutazama vile Mungu anaweza kuwa mwenye haki wakati anahesabia haki mwenye zambi anayetubu.TSHM 199.1

    Kazi ya Kristo kama mutetezi wa binadamu, inafananishwa katika Zakaria: “Atajenga hekalu la Bwana; na atachukua utukufu, na atakaa na kutawala juu ya kiti chake [cha Baba] cha enzi; naye atakuwa kuhani kwa enzi yake, na mshauri wa amani atakuwa katikati yao wawili”. Zacharia 6:12,13.TSHM 199.2

    “Atajenga hekalu la Bwana”. Kwa zabihu yake na upatanisho, kristo ni msingi na mjengaji wa kanisa la Mungu, “jiwe kubwa la pembeni. Katika yeye jengo lote linaunganishwa vema na kukaa hata liwe hekalu takatifu katika Bwana”. Waefeso 2:20,21. “Atachukua utukufu”. Wimbo wa wale watakaonunuliwa utakuwa: “kwake yeye aliyetupenda na kutuosha zambi zetu kwa damu yake,...kwa yeye utukufu na uwezo hata milele na milele”. Ufunuo 1:5,6.TSHM 199.3

    Atakaa na kutawala juu ya kiti chake cha enzi; naye atakuwa kuhani juu ya kiti chake cha ufalme”. Ufalme wa utukufu haujaingiliwa bado. Mpaka kazi yake kama mpatanishi imalizike, ndipo Mungu atamtolea ufalme ambao “hautakuwa na mwisho” Luka 1:33. Kama kuhani, Kristo anakaa sasa pamoja na Baba katika kiti chake cha enzi. Juu ya kiti kile cha ufalme kunakuwa yeye “aliyechukua taabu zetu; na kubeba huzuni zetu”, ambaye alikuwa “katika mambo yote alijaribiwa sawa sawa na sisi, lakini pasipo kufanya zambi”, kusudi aweze kusaidia wale wanaojaribiwa”. Isaya 53:4; Waebrania 4:15; 2:18. Mikono iliyojeruhiwa, upande uliochomwa mukuki,nya yo ilioharibiwa, vinamtetea mwanadamu aliye anguka ambaye wokovu wake ulipatikana kwa bei sawa ile.TSHM 199.4

    “Na shauri la salama litakuwa katikati ya wale wawili”. Upendo wa Baba ni chemchemi ya wokovu kwa ukoo uliopotea. Yesu aliwaambia wafuasi wake, “Baba yeye mwenyewe anawapenda”. Mungu alikuwa “ndani ya Kristo akipatanisha ulimwengu naye mwenyewe”. “Mungu alipenda ulimwengu hata kutoa Mwana wake wa pekee”. Yoane 16:27; 2 Wakorinto 5:19; Yoane 3:16.TSHM 199.5

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents