Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents
Tangu Sasa Hata Milele - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    1 / UNABII WA HALI YA MWICHO WA ULIMWENGU

    Kutoka kwa kilele cha Mizeituni, Yesu akatazama juu ya Yerusalema. Mbele ya makutano kulikuwa na majengo mazuri ya hekalu. Kushuka kwa jua kukaangazia weupe wa teluji wa kuta zake za marimari na kumulikia mnara wa zahabu na mnara mrefu mwembamba (Pinnacle). Mtoto gani wa Israeli aliweza kutazama juu ya maajabu haya bila kufurahi sana na kushangaa! Lakini mawazo mengine yalikuwa moyoni mwa Yesu. “Naye alipokaribia, akaona muji, akalia juu yake”. Luka 19:41.TSHM 1.1

    Machozi ya Yesu haikuwa kwa ajili yake mwenyewe, ingawa mbele yake kulikuwa Getesemane, mambo ya maumivu makubwa yaliyokaribia, na si mbali sana na, Kalvari, mahali pa kusulubiwa. Lakini haikuwa mambo hayo yaliyotia kivuli juu yake katika saa hii ya furaha. Alilia kwa ajili ya maelfu ya watu wa Yerusalema watakaoangamizwa.TSHM 1.2

    Historia ya zaidi ya miaka elfu ya upendeleo wa kipekee wa Mungu na ulinzi mkubwa, ulifunuliwa kwa watu wachaguliwa, ilifunguliwa kwa macho ya Yesu. Yerusalema uliheshimiwa na Mungu juu ya dunia yote. Bwana “amechagua Sayuni ... kuwa kao lake”. Zaburi 132:13. Kwa miaka mingi, manabii watakatifu walikuwa wakitoa ujumbe wa maonyo. Siku kwa siku damu ya wana kondoo ilikuwa ikitolewa, ikionyesha Mwana Kondoo wa Mungu.TSHM 1.3

    Israeli kama taifa angalilinda utii wake kwa Mungu, Yerusalema ungalisimama milele, mchaguliwa wa Mungu. Lakini historia ya wale watu waliopendelezwa ilikuwa habari ya kukufuru na kuasi. Zaidi kuliko upendo wa huruma wa baba, Mungu alikuwa mwenye “huruma kwa watu wake na makao yake”. 2 Mambo 36:15. Wakati maombi na makaripio yaliposhindwa, alituma zawadi bora sana ya mbinguni, Mwana wa Mungu Mwenyewe, kwa kutetea pamoja na muji usiotubu wa moyo mgumu.TSHM 1.4

    Kwa miaka mitatu Bwana wa nuru na utukufu alikuwa akiingia na kutoka miongoni mwa watu wake. “Akifanya kazi njema na kuponyesha wote walioonewa na Shetani”. Kuhubiri wokovu kwa wafungwa, na vipofu kupata kuona tena, kuwezesha viwete kutembea, na viziwi kusikia, kutakasa wenye ukoma, kufufua wafu, na kuhubiri Habari Njema kwa masikini. Tazama Matendo 10:38; Luka 4:18; Matayo 11:5.TSHM 1.5

    Mtembezi asiye na makao, aliishi kwa kusaidia wenye mahitaji na kupunguza misiba ya watu, kuwasihi kukubali zawadi ya uzima. Mawimbi ya huruma yaliyopingwa na waie waliokuwa na mioyo migumu, yakarudia na mwendo wa nguvu wa huruma, upendo usioelezeka. Lakini Israeli akamuacha Rafiki wake mwema na Msaidizi wa pekee. Maombezi ya upendo wake yakazarauliwa.TSHM 2.1

    Saa ya tumaini na musamaha ilikuwa ikipita upesi. Wingu lile ambalo lilikuwa likijikusanya katika miaka ya kukufuru na kuasi ilikuwa karibu kupasuka juu ya watu wenye kosa. Yeye ambaye peke yake alipashwa kuwaokoa kwa hatari yao ya kifo amezarauliwa, kutukanwa, kukataliwa, na alikuwa karibu kusulubiwa.TSHM 2.2

    Kristo alipotazama Yerusalema, mwisho wa muji mzima, taifa lote, ulikuwa mbele yake. Alisikia malaika mwangamizi pamoja na upanga ulioinuka juu ya mji ambao ulikuwa kwa wakati mrefu makao ya Mungu. Katika mahali palepale ambapo baadaye pakashikwa na Tito na jeshi lake, akatazama kwa bonde viwanja vitakatifu na mabaraza. Na machozi machoni akaona kuta kuzungukwa na majeshi ya kigeni. Alisikia shindo la jeshi kutembea kwa vita, sauti za wamama na watoto walililia mkate ndani ya muji uliozungukwa. Aliona nyumba yake takatifu, majumba yake na minara, yakitolewa kwa ndimi za moto, fungu la kuharibika lenye kuwaka na kutoka moshi.TSHM 2.3

    Kutazama katika nyakati, aliona watu wa ahadi kutawanyika katika kila inchi, “kama mavunjiko ya merikebu kwa pwani ya ukiwa”. Huruma ya Mungu, upendo mkuu, yakapata usemi katika maneno ya kusikitisha: “Ee Yerusalema, unaoua manabii, na kuwapiga kwa mawe wale waliotumwa kwako! Ni mara ngapi nimetaka kukusanya watoto wako pamoja, kama vile kuku anavyokusanya watoto wake chini ya mabawa yake, lakini ninyi hamukutaka”! Matayo 23:37.TSHM 2.4

    Kristo aliona katika Yerusalema mfano wa ulimwengu uliokazana katika kutoamini na kuasi, ukijiharakisha kwa kukutana na hukumu za kulipiza kisasi cha Mungu. Moyo wake ukashikwa na huruma kwa ajili ya waliohuzunishwa na walioteswa na dunia. Alitamani sana kuwafariji wote. Alitaka kutoa roho yake kwa kifo kwa kuleta wokovu karibu nao.TSHM 2.5

    Mtukufu wa mbinguni katika machozi! Mambo ile huonesha namna gani ni vigumu kuokoa mwenye kosa kwamatokeo ya kuharibu sheria ya Mungu. Yesu aliona ulimwengu kujitia katika madanganyo kama yale ambayo yalileta uharibifu wa Yerusalema. Zambi kubwa ya Wayahudi ilikuwa ni kukataa Kristo; zambi kubwa ya ulimwengu ingekuwa kukataa sheria ya Mungu, msingi wa serekali yake katika mbingu na dunia. Mamilioni katika utumwa wa zambi,ambao watahukumiwa kwa mauti ya pili, waliweza kukataa kusikiliza maneno ya kweli katika siku yao ya hukumu.TSHM 2.6

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents