Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents
Tangu Sasa Hata Milele - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    Utakaso wa Biblia

    Utakaso unahusu hali kamili ya mtu--roho, nafsi, na mwili. Tazama 1 Watesalonika 5:23. Wakristo wanaalikwa kutoa miili yao, “iwe zabihu iliyo hai, takatifu, ya kupendeza Mungu.” Waroma 12:1. Kila desturi yo yote inayozoofisha nguvu za mwili ao akili inaondolea mtu uwezo kwa kazi ya Muumba. Wale wanaompenda Mungu kwa moyo wao wote watatafuta daima kuleta nguvu zote za maisha yao kwa umoja pamoja na sheria zinazoendeleza nguvu zao kwa kufanya mapenzi yake. Hawatalegeza wala kuchafua sadaka wanayotoa kwa Baba wao wa mbinguni kwa anasa ya tamaa wala ulafi.TSHM 229.1

    Furaha yote ya zambi inaelekea kuzoofisha na kuua fahamu za akili na za kiroho; Neno wala Roho ya Mungu inaweza kufanya mguso mdogo kwa moyo. “Tujisafishe wenyewe kwa uchafu wote wa mwili na wa roho, tukitimiza utakatifu katika woga wa Mungu.” 2 Wakorinto 7:1.TSHM 229.2

    Ni wangapi wanaojitangaza kuwa Wakristo wanaoharibu sura yao ya kimungu kwa ulafi, kwa kunywa mvinyo, kwa anasa zilizokatazwa. Na kanisa vivyo hivyo hushawishi uovu, kwa kujaza tena mali yake ambayo mapendo kwa Kristo ni zaifu sana kutoa. Kama Kristo angeingia kwa makanisa ya leo na kutazama karamu iliyofanywa pale kwa jina la dini, je, hangalifukuza wale wakufuru, kama alivyofukuzia mbali wabadili feza kwa hekalu?TSHM 229.3

    “Hamujui ya kuwa mwili wenu ni hekalu la Roho Mtakatifu aliye ndani yenu, muliyepewa na Mungu? Na ninyi si mali yenu wenyewe; kwa sababu mulinunuliwa kwa bei; basi tukuzeni Mungu katika mwili wenu na katika roho yenu, maana ni ya Mungu.” 1 Wakorinto 6:19,20. Yeye ambaye mwili wake ni hekalu la Roho Mtakatifu hatafanywa mtumwa wa desturi mbaya. Nguvu zake ni za Kristo. Mali yake ni ya Bwana. Namna gani angetapanya hazina uliyo gabiziwa?TSHM 229.4

    Wanaojitangaza kuwa Wakristo kila mwaka wanatumia feza nyingi kwa anasa mbaya. Mungu wanamuiba kwa zaka na sadaka, wanapoteketeza kwa mazabahu ya tamaa mbaya ya kuharibu zaidi kuliko wanavyotoa kwa kusaidia maskini ao kusaidia maendeleo ya habari njema. Kama wote wanaoshuhudia Kristo wangetakaswa kwa kweli, mali yao, badala ya kuitumia kwa anasa za bure na zenye hasara, yangerudishwa katika hazina ya Bwana. Wakristo wangetoa mufano wa kiasi na kujitoa kafara. Ndipo wangekuwa nuru ya ulimwengu.TSHM 229.5

    “Tamaa ya mwili, na tamaa ya macho, na kiburi cha maisha” (1 Yoane 2:16) zinatawala wingi wa watu. Lakini wafuasi wa Kristo wanakuwa na mwito takatifu. “Tokeni katikati yao, mukatengwa nao, Bwana anasema, wala musiguse kitu kisicho safi.” Kwa wale wanaokubali pamoja na mapatano, ahadi za Mungu ni “Nitakuwa baba kwenu, nanyi mutakuwa kwangu wana na binti, Bwana Mwenyezi anasema.” 2 Wakorinto 6:17,18.TSHM 230.1

    Kila hatua ya imani na utii inaleta nafsi kwa uhusiano wa karibu sana na Nuru ya Ulimwengu. Mwangaza safi wa Jua la Haki unaangazia juu ya watumishi wa Mungu, na wanapaswa kurudisha mishale ya nuru yake. Nyota zinatwambia kwamba hapo kuna nuru katika mbingu na kwa utukufu wake zinangaa; kwa hivi Wakristo wanaonyesha kwamba hapo kuna Mungu kwa kiti cha enzi ambaye tabia yake ni bora ya sifa na ya kuiga. Utakatifu wa tabia yake utaonyeshwa katika ushuhuda wake.TSHM 230.2

    Katika sifa njema za Kristo tunakuwa na ruhusa ya kukaribia kwa kiti cha Mwenye uwezo usio na mwisho (Mungu). “Yeye asiyeachilia Mwana wake, lakini alimutoa kwa ajili yetu zote, namna gani atakosa kututolea vitu vyote pamoja naye?” Yesu asema: “Kama ninyi mulio wabaya munajua kuwapa watoto wenu zawadi njema, si zaidi Baba yenu aliye katika mbingu atawapa wote wanaomwomba Roho Mtakatifu?” “Kama mukiomba neno gani kwa jina langu, nitalifanya.” “Mwombe, na mutapata, furaha yenu itimizwe.” Waroma 8:32; Luka 11:13; Yoane 14:14; 16:24.TSHM 230.3

    Ni heshima ya kila mumoja kuishi ambako Mungu atakao kubali na kubarikia. Si mapenzi ya Baba yetu wa mbinguni ya kuwa tupate kuwa chini ya hukumu na giza. Hapo hakuna ushuhuda wa unyenyekevu wa kweli katika kwenda pamoja na kichwa cha kuinama chini na moyo unaojaa na mawazo ya uchoyo. Tunaweza kwenda kwa Yesu na kutakaswa na kusimama mbele ya sheria pasipo haya na majuto.TSHM 230.4

    Katika Yesu wana wa Adamu walioanguka wanakuwa “wana wa Mungu.” Kwa sababu hii haoni haya kuwaita ndugu zake.” Maisha ya mkristo yanapaswa kuwa yale ya imani moja, ushindi, na furaha katika Mungu. “Maana furaha ya Bwana ni nguvu zenu.” “Furahini siku zote. Ombeni pasipo kuacha. Katika maneno yote mushukuru; maana maneno haya ni mapenzi ya Mungu kwenu katika Kristo Yesu.” Waebrania 2:11; Nehemia 8:10; 1 Watesalonika 5:16-18.TSHM 230.5

    Haya ndiyo yanavyokuwa matunda ya toba ya Biblia na utakaso; na ni kwa sababu ya kanuni kubwa za haki zilizo wekwa katika sheria zinaangaliwa kwa kutojali kwamba matunda haya yanashuhudiwa kwa shida. Hii ndiyo sababu hapo kunaonyeshwa kidogo sana kazi nyingi ile, yenye kudumu ya Roho ambayo iliyoonyesha maamsha ya kwanza.TSHM 230.6

    Ni kwa kutazama ile tunakuwa wenye kubadilika. Wakati amri hizo takatifu ambamo Mungu amefungulia watu ukamilifu na utakatifu wa tabia yake zimezarauliwa, na akili za watu zimevutwa kwa mafun-disho na maelezo ya watu, hapo kulifuatwa na upungufu wa utawa katika kanisa. Ni wakati tu sheria ya Mungu imerudishwa kwa hali yake ya haki ndipo pale panaweza kuwa na muamsho wa imani ya zamani za kwanza na utawa miongoni mwa watu wake wanaojulikana.TSHM 231.1

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents