Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents
Tangu Sasa Hata Milele - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    Maandiko matakatifu na Taratibu ya Miaka

    Haya pamoja na maandiko mengine kwa wazi yakamshuhudia Miller kwamba utawala wa amani wa watu wote na kuimarishwa kwa ufalme wa Mungu duniani ungekuwa baada ya kuja kwa mara ya pili. Tena, hali ya ulimwengu ililingana na maelezo ya unabii wa siku za mwisho. Alilazimishwa kwa mwisho kwamba mda uliogawanywa kwa dunia katika hali yake ya sasa ulikuwa karibu kuisha.TSHM 153.3

    Namna ingine ya ushuhuda ambao kwa nguvu ulichoma moyo wangu.” Akasema, “ulikuwa utaratibu wa Maandiko... Niliona kwamba mambo yaliyotabiriwa, yalitimilika katika wakati uliopita, mara kwa mara yalitukia karibu ya wakati uliotolewa... Matokeo ... yanapokuwa tu mambo ya unabii, ... yalitimia katika upatano wa yale yaliotabiriwa.”TSHM 153.4

    Wakati alipoona nyakati za taratibu ya miaka ambayo ilifikia kwa kuja kwa mara ya pili kwa Kristo, hangaliweza lakini kuzitazama kama “nyakati zilizoonyeshwa mbele”, ambazo Mungu alifunulia watumishi wake. “Vitu vile vilivyofunuliwa ni vyetu, na vya wana wetu milele.” Bwana alitangaza kwamba “hatafanya lolote, lakini anafunulia watumishi wake manabii siri yake.” Torati 29:29; Amosi 3:7. Wanafunzi wa Neno la Mungu wanaweza kutazamia kwa hakika kuona mambo makubwa kuliko katika historia ya wanadamu iliyoonyeshwa kwa wazi katika Maandiko.TSHM 153.5

    “Nilisadikishwa kabisa,” akasema Miller, “kwamba kila andiko lililopewa kwa maongozi ya Mungu linafaa kwa mafundisho; kwamba liliandikwa; wakati watu watakatifu walikuwa wakiongozwa na Roho Mtakatifu, yameandikwa kwa majifunzo yetu, kwamba kwa subira na faraja ya maandiko tuwe na tumaini ... kwa hiyo mimi niliona kwamba katika kujitahidi kufahamu kile Mungu alikuwa nacho katika huruma zake kinachoonekana kufaa kwa kufunuliwa kwetu, sikuwa na haki kupita inje ya nyakati za unabii.”TSHM 154.1

    Unabii ambao ulionekana wazi zaidi kwa kufunua wakati wa kuja kwa mara ya pili ulikuwa Danieli 8:14: “Hata mangaribi na asubui elfu mbili mia tatu; halafu Pahali patakatifu patasafishwa.” Kufanya Maandiko mfasiri wake mwenyewe, Miller akajifunza kwamba siku moja katika unabii ni mwaka moja. (Tazama Nyongezo.) Aliona kwamba siku 2300 za unabii, ao miaka kabisa, ingefikia mbali sana ya mwisho wa mugawo wa Wayahudi, kwa hiyo haikuweza kutaja juu ya mahali patakatifu pa mugawo ule.TSHM 154.2

    Miller akakubali maelezo ya kawaida kwamba katika miaka ya Kikristo ulimwengu ni “mahali patakatifu,” na kwa hiyo akafahamu kwamba kusafishwa kwa mahali patakatifu kulikotabiriwa katika Danieli 8:14 ilikuwa mfano wa kutakaswa kwa dunia na moto kwa kuja kwa mara ya pili kwa Kristo. Kama mahali kamili pa kuanzia pangeweza kupatikana kwa ajili ya siku 2300, akamaliza kwamba wakati wa kuja kwa mara ya pili ungeweza kufunuliwa.TSHM 154.3

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents