Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents
Tangu Sasa Hata Milele - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    Masharti Yameelezwa

    “Mimi nitamupa yeye mwenye kiu, ya chemchemi ya maji ya uzima, bure.” Ahadi hii ni ya wale tu wanaokuwa na kiu. “Yeye anayeshinda atariti maneno haya, nami nitakuwa Mungu wake, naye atakuwa mwana wangu.” Ufunuo 21:6,7. Mashairi yameelezwa. Kwa kuriti vitu vyote, inatupasa kushinda zambi.TSHM 263.3

    “Lakini haitakuwa heri kwake mwovu.” Muhubiri 8:13. Mwenye zambi anajiwekea mwenyewe “hasira kwa siku ya hasira na ufunuo wa hukumu ya haki ya Mungu, atakayelipa kila mutu kwa kadiri ya matendo yake;” “mateso na taabu juu ya kila nafsi ya mutu anayefanya uovu.” Waroma 2:5,6,9.TSHM 263.4

    “Hakuna mwasherati wala mutu muchafu wala mwenye tamaa, ndiye mwabudu sanamu, aliye uriti katika ufalme wa Kristo na Mungu.” “Heri wale wanaofula nguo zao, wawe na amri kwendea mti wa uzima, na kuingia katika muji kwa milango yake. Lakini inje ni imbwa, na wachawi, na wazini, na wauaji, na wanaoabudu sanamu, na kila mutu anayependa uwongo na kuufanya.” Waefeso 5:5, ARV; Ufunuo 22:14,15.TSHM 263.5

    Mungu amewatolea watu tangazo la kanuni ya matendo na zambi. “Waovu wote atawaharibu.” ‘’Lakini wakosaji wataharibiwa pamoja; mwisho wa waovu utaharibiwa.” Zaburi 145:20; 37:38. Mamlaka ya serikali ya Mungu itaharibu maasi, lakini haki ya kulipiza kisasi itakuwa aminifu pamoja na tabia ya Mungu kama wa rehema, na wema.TSHM 264.1

    Mungu hashurutishe mapenzi. Hapendezwi na utii wa utumwa. Anataka ya kama viumbe vya mikono yake watampenda kwa sababu anastahili upendo. Angaliwatakia wamtii kwa sababu wanakuwa na shukrani ya akili kwa hekima yake, haki, na wema.TSHM 264.2

    Kanuni za serkali ya Mungu zinakuwa katika umoja pamoja na amri ya Mwokozi, “Pendeni adui zenu.” Matayo 5:44. Mungu anatimiliza haki kwa waovu kwa ajili ya uzuri wa viumbe vyote na hata kwa ajili ya uzuri wa wale ambao hukumu zake zitakapowatazama. Angewafurahisha kama awezavyo. Amewazunguusha na alama za upendo wake na kuwafuatisha na matoleo za rehema; lakini wanazarau upendo wake, wanavunja sheria yake, na kukataa rehema yake. Kupokea daima zawadi zake, wanampatisha haya Mtoaji. Bwana anavumilia ukaidi wao wakati mrefu; lakini je, atawafunga waasi hawa kwa upande wake, kuwalazimisha kufanya mapenzi yake?TSHM 264.3

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents