Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents
Tangu Sasa Hata Milele - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    Damani (Bei) ya Mafundisho ya Ukweli

    Mafundisho ya ukweli yalikuwa na bei kuliko nyumba na inchi, rafiki, jamaa, hata maisha yenyewe. Kutokea mwanzo wa utoto, vijana walifundishwa kuheshimu maagizo matakatifu ya sheria ya Mungu. Kurasa za Biblia zilikuwa chache; kwa hiyo maneno yake ya damani yaliwekwa kwa uwezo wa kukumbuka. Wengi waliweza kukariri sehemu nyingi za Agano la Kale na Agano Jipya.TSHM 23.4

    Walifundishwa toka utoto kuvumilia ugumu na kufikiri na kutenda kwa ajili ya wao wenyewe. Walifundishwa kuchukua madaraka, kujilinda kwa usemi, na kufahamu hekima ya utulivu. Neno moja la ujinga linaposikiwa kwa maadui wao lingeweza kuleta hasara ya maisha ya mamia ya wandugu, kwani kama vile mbwa mwitu katika kuwinda mawindo, maadui wa kweli wanawinda wale waliosubutu kutangaza uhuru wa imani ya dini.TSHM 24.1

    Wavaudois kwa uvumilivu walitaabika kwa ajili ya chakula chao. Kila mahali padogo pa udongo wa kulimiwa katikati ya milima palitumiwa vizuri. Kiasi katika utumizi wa feza na kujikana yakafanya sehemu ya elimu yao ambayo watoto walijifunza. Kazi ilikuwa ya taabu lakini yakufaa kwa afya, basi ndicho mtu anachohitaji katika hali yake ya kuanguka. Vijana walifundishwa kwamba nguvu zao zote ni za Mungu, zipate kusitawishwa kwa ajili ya kazi yake.TSHM 24.2

    Makanisa ya Wavaudois yalifanana na kanisa la nyakati za mitume. Kukataa mamlaka ya Papa na askofu, walishika Biblia kuwa na mamlaka yasiyoweza kukosa. Wachungaji wao, hawakufanana na mapadri wa kiburi wa Roma, wakalisha kundi la Mungu, kuwaongoza katika malisho ya majani mabichi na chemchemi ya Neno takatifu lake. Watu walikusanyika si ndani ya makanisa ya maridadi ao makanisa makuu ya majimbo, bali katika mabonde ya Milima mirefu, ao, katika wakati wa hatari, ndani ya ngome ya miamba, kwa kusikiliza maneno ya ukweli kutoka kwa watumishi wa Kristo. Wachungaji hawakuhubiri injili tu, walizuru wagonjwa na wakatumika kwa kuamusha umoja na upendo wa ndugu. Kama Paulo fundi wa kufanya hema, kila mmoja wao alijifunza kazi fulani ambayo kwayo, kama ni lazima, kingemusaidia kwa kujitegemea mwenyewe.TSHM 24.3

    Vijana walipata mafundisho yao kwa wachungaji wao. Biblia ilifanywa kuwa masomo ya mhimu. Injili za Matayo na Yoane ziliwekwa katika ukumbusho, pamoja na barua nyingine.TSHM 24.4

    Mara zingine katika mapango ya giza udongoni, kwa nuru ya mienge (torches), Maandiko matakatifu yaliandikwa, mstari kwa mstari. Malaika kutoka mbinguni wakazunguuka watumishi hawa waaminifu.TSHM 24.5

    Shetani alilazimisha mapadri wa Papa na maaskofu kuzika Neno la Ukweli chini ya machafu ya makosa na ibada ya uchawi. Lakini kwa namna ya ajabu likalindwa bila kuchafuliwa wakati wa miaka yote ya giza. Kama safina juu ya mawimbi mazito, Neno la Mungu linashinda zoruba zinazolitisha kuliharibu. Kama vile dini yamefikia bamba la jiwe lenye zahabu na feza iliyofichwa chini upande wa juu, ni vivyo hivyo Maandiko matakatifu yanakuwa na hazina ya ukweli iliyofunuliwa tu kwa wanyenyekevu, wanaopenda kuomba Mungu alichagua Biblia kuwa kitabu cha mafundisho ya wanadamu wote kuwa ufunuo wake mwenyewe. Kila ukweli uliotambuliwa ni uvumbuzi mupya wa tabia ya Mwandishi wake.TSHM 24.6

    Kutoka kwa vyuo vyao katika milima vijana wengine walitumwa kujifunza katika Ufaransa ao Italia, ambapo palikuwa na nafasi kubwa zaidi kwa mafundisho na uchunguzi kuliko katika inchi yao ya milima mirefu. Vijana waliotumwa walijihatarisha kwa majaribu. Walipambana na wajumbe wa Shetani waliowalazimisha mambo ya kipinga ukweli wa dini na madanganyo ya hatari. Lakini elimu yao tokea utoto ikawatayarisha kwa jambo hili.TSHM 25.1

    Katika vyuo po pote walipokwenda hawakuweka tumaini lao kwa kitu cho chote. Mavazi yao yalitayarishwa kama kuficha hazina zao kubwa-Maandiko. Mara kwa mara walivyoweza waliweka kwa uangalifu sehemu za maandiko njiani mwa wale ambao mioyo yao ilionekana kufunguliwa kwa kupokea ukweli. Waiiotubu na kukubali imani ya kweli walipatikana katika vyuo hii vya elimu, mara kwa mara mafundisho ya imani ya kweli ikaenea kwa chuo chote kizima. Huku waongozi wa Papa hawakuweza kupata mwanzo wa kile walichoitwa “Upinzani wa mafundisho ya dini”.TSHM 25.2

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents