Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents
Tangu Sasa Hata Milele - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    Ujushi wa Maumivu Mabaya ya Milele

    Uovu ulifanyika kwa sababu ya ujushi wa maumivu mabaya ya milele. Dini ya Biblia, inajaa na upendo na wema, inatiwa giza kwa imani ya mambo ya uchawi na inavikwa na hofu kubwa. Shetani amepakaa rangi tabia ya Mungu kwa rangi za uwongo. Muumba wetu wa rehema anaogopwa, na kuhofiwa, hata kuchukiwa. Maoni ya kutisha ya Mungu ambayo yameenea po pote ulimwenguni kutoka kwa mafundisho ya mimbara yamefanya mamilioni ya watu wenye mashaka na wasiokuwa waaminifu.TSHM 262.2

    Maumivu mabaya ya milele ni mojawapo ya mafundisho ya uwongo, mvinyo wa gazabu yake (Ufunuo 14:8; 17:21), ambayo Babeli inafanya wote kunywa. Wahuduma wa Kristo walipokea ujushi huu kwa Roma kama walivyokubali sabato ya uwongo. Kama tukiacha Neno la Mungu na kukubali mafundisho ya uwongo kwa sababu wababa zetu waliyafundisha, tunaanguka chini ya hukumu iliyotangazwa kwa Babeli; tunakunywa mvinyo wa gazabu yake.TSHM 262.3

    Kundi kubwa linaongozwa kwa kosa la upande mwingine. Wanaona Maandiko yanayoonyesha Mungu kama mwenye upendo na huruma na hawawezi kuamini kwamba atatupa viumbe kwa jehanum inayowaka milele. Kushikilia kwamba nafsi kwa kawaida ni ya milele, wakaishia kwamba watu wote wataokolewa. Kwa hivyo mwenye zambi anaweza kuishi katika anasa ya kupendeza nafsi, kutojali matakwa ya Mungu, na kukubaliwa na Mungu. Mafundisho ya namna hiyo, yanategemea kwa rehema ya Mungu lakini bila kujali haki yake, yanafurahisha moyo wa tamaa za mwili.TSHM 262.4

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents