Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents
Tangu Sasa Hata Milele - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    Makutano Huko Augsburg

    Watawala wa injili walinyimwa kusikiwa na Mfalme Ferdinand, lakini kwa kutuliza magomvi yaliyosumbua ufalme, Charles V katika mwaka uliofuata Ushuhuda wa Spires akaita makutano huko Augsburg. Akatangaza kusudi lake kwa kuongoza mwenyewe. Waongozi wa Kiprotestanti wakaitwa.TSHM 94.3

    Mchaguzi wa Saxony akashurutishwa na washauri wake asionekane kwa makutano: “Je, hivyo si kujihatarisha kwa kwenda kwa kila kitu na kujifungia ndani ya kuta za muji pamoja na adui wenye nguvu?” Lakini wengine wakamwambia kwa uhodari “Acha watawala tu wapatane wao wenyewe na uhodari na hoja ya Mungu itaokoka.” “Mungu ni mwaminifu: hatatuacha,” akasema Luther.TSHM 94.4

    Mchaguzi akashika safari kwenda Augsburg. Wengi wakaenda kwenye mkutano na uso wa huzuni na moyo wa taabu. Lakini Luther aliyewasindikiza hata Coburg, akaamsha imani yao kwa kuimba wimbo ulioandikwa walipokuwa safarini, “ngome yenye uwezo ndiye Mungu wetu’. Mioyo nyingi yenye uzito ikawa nyepesi kwa sauti za juhudi za kutia moyo.TSHM 94.5

    Watawala walioongoka wakakusudia kuwa na maelezo ya maono yao, pamoja na ushuhuda kutoka kwa Maandiko, ya kuonyesha mbele ya mkutano. Kazi ya matayarisho yake ikapewa Luther, Melanchton na washiriki wao. Ungamo hili likakubaliwa na Waprotestanti, na wakakusanyika kwa kutia majina yao kwa maandiko ya mapatano.TSHM 95.1

    Watengenezaji walitamani zaidi bila kuchanganisha hoja yao na maswali ya siasa. Kama vile watawala Wakikristo waliendelea kutia sahihi ya ungamo, Melanchton akaingia kati, na kusema, “Ni kwa wachunguzi wa mambo ya dini na wahubiri kwa kutoa shauri la mambo haya; tuchunge maoni mengine kwa ajili ya mamlaka ya wakuu wa inchi.” “Mungu anakataza” akajibu Jean wa Saxony, “Kwamba mgenitenga. Ninakusudia kutenda yaliyo haki, bila kujihangaisha mimi mwenyewe juu ya taji langu. Natamani kuungama Bwana. Kofia yangu ya uchaguzi na ngozi ya mapendo ya wahukumu si vya damani kwangu kama msalaba wa Yesu Kristo.” Akasema mwengine katika watawala alipochukua kalamu, “Kama heshima ya Bwana wangu Yesu Kristo huidai, niko tayari ... kuacha mali na maisha yangu nyuma.” “Tafazali ningekataa mambo yangu na makao yangu, zaidi kutoka inchini mwa baba zangu na fimbo mkononi,” akaendelea, “kuliko kukubali mafundisho mengine mbali na ambayo yanayokuwa katika ungamo hili.”TSHM 95.2

    Wakati ulioagizwa ukafika. Charles V, akazungukwa na wachaguzi na watawala, akakubali kuonana na Watengenezaji wa Waprotestanti. Katika mkutano tukufu ule mambo ya kweli ya injili yakatangazwa wazi wazi na makosa ya kanisa la Papa yakaonyeshwa. Siku ile ikatangazwa “siku kubwa sana ya Matengenezo, na siku mojawapo ya utukufu katika historia ya Kikristo na ya wanadamu.”TSHM 95.3

    Mtawa wa Wittenberg akasimama peke yake huko Worms. Sasa mahali pake kukawa watawala hodari kuliko wa ufalme. “Ninafurahi sana,” Luther akaandika, “kwamba nimeishi hata kwa wakati huu, ambao Kristo ametukuzwa wazi wazi na mashahidi bora kama hawa, na katika mkutano tukufu sana.”TSHM 95.4

    Ujumbe ambao mfalme alioukataza kuhubiriwa kwa mimbara ukatangazwa kwa jumba lake la kifalme. Maneno ambayo wengi waliifikiri kama yasiyofaa hata mbele ya watumikaji, yalisikiwa kwa mshangao na mabwana wakubwa na watawala wa ufalme. Wafalme walikuwa wahubiri, na mahubiri yalikuwa kweli aminifu ya Mungu. “Tangu wakati wa mitume hapakuwa kazi kubwa kuliko, ao maungamo mazuri zaidi.”TSHM 95.5

    Mojawapo ya kanuni imara zaidi iliyoshikwa nguvu na Luther ilikuwa kwamba haifae kutumainia uwezo wa kidunia katika kusaidia Matengenezo. Alifurahi kwamba injili ilitangazwa na watawala na ufalme; lakini wakati walipokusudia kuungana katika chama cha utetezi, akatangaza kwamba “mafundisho ya injili itatetewa na Mungu peke yake. ... Uangalifu wote wa siasa uliokusudiwa ulikuwa katika maoni yake, kwamba ulitolewa na hofu isiyofaa na shaka ya zambi.”TSHM 95.6

    Kwa tarehe ya baadaye, kufikiri juu ya mapatano yaliyoazimiwa na Wafalme walioongoka, Luther akatangaza kwamba silaha ya pekee tu katika vita hii inapashwa kuwa “upanga wa Roho.” Akaandika kwa mchaguzi wa Saxony: “Hatuwezi kwa zamiri yetu kukubali mapatano yaliyokusudiwa. Msalaba wa Kristo unapaswa kuchukuliwa. Hebu utukufu wako uwe bila hofu. Tutafanya mengi zaidi kwa maombi yetu kuliko maadui wetu wote kwa majivuno yao.”TSHM 96.1

    Kutoka kwa pahali pa siri pa sala kukaja uwezo uliotetemesha ulimwengu katika Matengenezo. Huko Augsburg Luther “hakupitisha siku bila kujitoa kwa maombi kwa masaa tatu.” Ndani ya chumba chake cha siri alikuwa akisikia kumiminika kwa roho yake mbele ya Mungu kwa maneno “yanayojaa na kuabudu na hofu na matumaini.” Kwa Melanchton akaandika: “Kama sababu si ya haki, tuiache; kama sababu ni ya haki, sababu gani kusingizia ahadi za yule anaye tuagiza kulala bila hofu?” Watengenezaji wa Kiprotestanti walijenga juu ya Kristo. Milango ya kuzimu haitalishinda!TSHM 96.2

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents