Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents
Tangu Sasa Hata Milele - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    Kuinuka kwa Mamlaka Mpya

    Kwa jambo hili mfano mwingine umetangazwa: “Kisha nikaona mnyama mwingine akipanda juu toka dunia, naye alikuwa na pembe mbili, mfano wa Mwana-Kondoo.” Ufunuo 13:11. Taifa hili ni mbalimbali na yale yaliyoonyeshwa chini ya mifano iliyotangulia. Falme kubwa zilizotawala dunia zilionyeshwa kwa nabii Danieli kama wanyama wa mawindo, waliopanda wakati “pepo ine za mbingu zilivuma kwa nguvu juu ya bahari kubwa.” Danieli 7:2. Katika ufunuo 17:15 malaika anaeleza kwamba maji yanafanyishwa na “Watu” na makutano ya mataifa na lugha”. Upepo ni mfano wa mashindano (vita). Pepo ne zinazo shindana juu ya bahari kubwa inaonyesha matendo ya hatari ya ushindi na wapinduzi ambayo falme zilifika kwa enzi.TSHM 212.2

    Lakini nyama aliyekuwa na pembe mfano wa Mwana-kondoo alionekana “akipanda toka dunia.” Badala ya kuangusha mamlaka zingine na kujiimarisha mwenyewe, taifa lililokuwa mfano wake lilipaswa kupanda katika inchi isiokaliwa kwanza na likasitawi kwa amani. Linapaswa kutafutwa katika Bara kuu la Magaribi.TSHM 212.3

    Ni taifa gani la Dunia Mpya lilikuwa katika mwaka 1798 likipanda kwa nguvu, kutoa ahadi ya nguvu, na kuvuta uangalifu wa dunia? Taifa moja, na ni moja tu, linalokutana na unabii huu--mataifa ya muungano ya Amerika (United States of America). Karibu sana maneno kabisa kabisa ya mwandishi mtakatifu yalitumiwa bila kufahamu kwa mwandishi wa historia katika kueleza kupanda kwa taifa. Mwandishi mashauri anasema juu ya “siri ya kutokea kwake kwa pahali patupu,” na anasema, “Kama mbegu ya kimya tunasitawi katika mamlaka.” Gazeti la Ulaya katika mwaka 1850 linaeleza juu ya Amerika “kutokea” na “katika utulivu wa inchi siku kwa siku kuongeza kwa uwezo wake na kiburi.”TSHM 212.4

    “Naye alikuwa na pembe mbili, mfano wa Mwana-Kondoo.” Pembe mfano wa mwana-kondoo inaonyesha ujana, hali ya kuwa bila kosa, upole. Miongoni mwa Wakristo wa kwanza waliokimbilia Amerika kwa ajili ya magandamizo ya kifalme na kutovumilia kwa mapadri kulikuwa wengi waliokusudia kuanzisha uhuru wa kiulimwengu na wa dini. Tangazo la uhuru linainua kweli kwamba “watu wote wameumbwa sawasawa” na wanatolewa na haki ya daima kwa “maisha, uhuru, na kutafuta furaha.” Sheria inatoa haki kwa watu ya kujitawala, kuhakikisha kwamba wajumbe waliochaguliwa kwa uchaguzi wa kupendwa na watu wote watafanya na kuamuru sheria. Uhuru wa imani ya dini ulitolewa pia. Utawala wa uchaguzi (Republicanism) ya Dini la Kiprotestanti yakawa kanuni za msingi za taifa, siri ya uwezo wake na usitawi. Mamilioni wakatafuta pwani zake, na Amerika ikapanda kwa pahali miongoni mwa mataifa yenye uwezo mwingi zaidi duniani.TSHM 212.5

    Lakini nyama aliyekuwa na pembe mbili, mfano wa mwanakondoo “akasema kama joka. Naye atumia uwezo wote wa mnyama yule wa kwanza mbele yake, na kufanya dunia nao wanaokaa ndani yake waabudu mnyama wa kwanza, ambaye kidonda chake cha mauti kilipona; ... akiwaambia wale wanaokaa juu ya dunia, kumfanyia sanamu yule mnyama, aliyekuwa na kidonda cha upanga, naye aliishi.” Ufunuo 13:11-14.TSHM 213.1

    Pembe mfano wa mwana-kondoo na sauti ya joka inaonyesha kwa mabishano. Utabiri kwamba itasema “kama joka” na kutumia “maneno kwa uwezo wote wa nyama yule wa kwanza” unatabiri roho ya kutokuwa na uvumilivu na ya kutesa. Na maneno kwamba mnyama aliyekuwa na pembe mbili “naye dunia alifanya” na wale wanaokaa ndani yake waabudu mnyama wa kwanza” inaonyesha kwamba mamlaka ya taifa hili ni kutumia nguvu kwa kushika maagizo fulani ambayo itakuwa tendo la heshima kwa utawala wa kipapa.TSHM 213.2

    Tendo la namna hiyo lingekuwa kinyume kwa asili ya sheria zake za uhuru, kwa taratibu ya maneno ya kukiri Tangazo la Uhuru, na kwa sheria. Sheria inaweka tayari kwamba “Baraza kuu haitaweka sheria kupendelea makao ya dini, wala kukataza uhuru wa matumizi hiyo,” na kwamba “hakuna jaribio la dini litakalodaiwa kamwe kama sifa kwa kazi yo yote ya tumaini la watu wote chini ya mataifa ya muungano (United States). Kuvunja wazi kwa kinga hizi (mambo yanayofanya salama) za uhuru kunaonyeshwa katika mfano huu. Mnyama aliyekuwa na pembe mbili mfano wa mwana-kondooanayejitangaza kuwa safi, mtulivu-asiyeumiza-anasema kama joka.TSHM 213.3

    “Akiwaambia wale wanaokaa juu ya dunia, kumfanyia sanamu yule nyama.” Hapa panaonyeshwa namna ya serkali ambapo mamlaka ya kufanya sheria inadumu kwa watu, ushuhuda wa kushangaza zaidi kwamba Amerika ni taifa lenye maana fulani.TSHM 213.4

    Lakini “sanamu kwa mnyama” ni nini? Namna gani inafanywa?TSHM 214.1

    Wakati kanisa la zamani lilipochafuka, likatafuta msaada wa uwezo wa kidunia. Matokeo: Kanisa la Roma (Papa), kanisa lililotawala serkali, hasa zaidi sana kwa ajili ya azabu ya uzushi.” Ili Amerika ipate kufanya ‘’sanamu ya mnyama,” mamlaka ya dini inapaswa kutongoza serkali kwamba serkali itatumiwa vilevile kwa kanisa kutimiza vifiko vyake mwenyewe.TSHM 214.2

    Makanisa ya Kiprotestanti yale yaliyofuata katika hatua za Roma yameonyesha mapenzi ya namna moja kwa kuzuia uhuru wa zamiri. Mfano ni mateso yaliyoendelea wakati mrefu ya wale wasiokubali mafundisho ya Kanisa la Kiingereza. Wakati wa karne za kumi na sita na kumi na saba, wachungaji na watu wasiokubali kanuni za kanisa walikuwa watu wakulipa feza ya azabu, kufungwa, mateso (azabu kali), na mauti ya mfia dini.TSHM 214.3

    Uasi ukaongoza kanisa la mwanzoni kutafuta usaada wa serkali ya raia. Na jambo hili likatayarisha njia kwa Kanisa la Roma (Papa)--mnyama. Paulo akasema: “ila maasi yale yafike mbele, na mtu yule wa kuasi akafunuliwa.” 2 Watesalonika 2:3.TSHM 214.4

    Biblia inatangaza: “Siku za mwisho zitakuwa nyakati za hatari. Kwa sababu watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda feza, wenye kujisifu, wenye kiburi, wenye kutukana, wasiotii wazazi wao, wasio na kushukuru, wasio safi, wasiopenda wenzao, wasiotaka kusamehe, washitaki wa uwongo, wasiojizuiza, wakali, wasiopenda mema, wadanganyifu, wakaidi, wenye kujivuna, wenye kupenda anasa kuliko Mungu; wenye mfano wa kuogopa Mungu, lakini wakikana nguvu zake.” 2 Timoteo 3:1-5. “Basi, Roho anasema waziwazi ya kwamba katika nyakati za mwisho watu wengine watajitenga na imani, wakisikiliza roho za kudanganya, na mafundisho ya mashetani.” 1 Timoteo 4:1.TSHM 214.5

    Wote wale “hawakupokea mapendo wa kweli, kwamba wapate kuokolewa,” watakubali “nguvu ya upotevu, hata waamini uwongo.” 2 Watesalonika 2:10,11. Wakati hali hii itakapofikiwa, matokeo ya namna moja yatafuata ilivyokuwa katika karne za kwanza.TSHM 214.6

    Tofauti kubwa ya imani katika makanisa ya Waprotestanti inazaniwa na wengi kama utibitizo kwamba hakuna umoja uliolazimishwa unaoweza kufanywa. Lakini pale kumekuwa kwa miaka nyingi katika makanisa ya Waprotestanti nia iliyoongezeka katika upendeleo wa umoja. Kwa kulinda umoja kama huo, mazungumzo ya mambo ambayo wote hawakuyakubali yanapaswa kuachwa kudaiwa. Katika bidii ya kulinda umoja kamili, itakuwa tu ni hatua kwa kutumia nguvu.TSHM 214.7

    Wakati makanisa maalum ya Amerika, yanapoungana juu ya mambo kama yale ya mafundisho kama inavyoshikwa kwao katika umoja, yatavuta serkali kulazimisha amri zao na kuimarisha sheria zao, ndipo Amerika ya Kiprotestanti itakapofanya sanamu ya serkali ya Kanisa la Roma, na azabu ya malipo ya raia juu ya wale wasiokubali mafundisho ya kanisa bila mashaka yatakuwa matokeo.TSHM 215.1

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents