Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents
Tangu Sasa Hata Milele - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    25 / SHERIA YA MUNGU ISIYOGEUKA

    “Hekalu la Mungu likafunguliwa mbinguni na sanduku ya agano lake likaonekana.” Ufunuo 11:19. Sanduku ya agano la Mungu linakuwa ndani ya Pahali patakatifu pa patakatifu, chumba cha pili cha Pahali patakatifu. Katika kazi ya hema ya duniani, ambayo ilitumiwa “katika mfano na kivuli cha vitu vya mbinguni,” chumba hiki kilikuwa kikifunguliwa tu kwa Siku kubwa ya Upatanisho kwa ajili ya usafisho wa Pahali patakatifu. Kwa hivyo tangazo kwamba hekalu la Mungu lilifunguliwa mbinguni na sanduku ya agano lake lilionekana linaonyesha kwa kufunguliwa kwa Pahali patakatifu pa patakatifu mno pa mbinguni katika mwaka 1844 ambapo Kristo aliingia kufanya kazi ya kumaliza upatanisho. Wale ambao katika imani walimufuata Kuhani wao Mkuu alipoingia kwa huduma yake katika Pahali patakatifu pa patakatifu mno, walitazama sanduku ya agano lake. Kwa namna walivyojifunza fundisho la Pahali patakatifu walipata kufahamu badiliko la kazi ya Mwokozi, na wakaona kwamba alikuwa sasa anahudumia mbele ya sanduku la Mungu.TSHM 209.1

    Sanduku ndani ya hema duniani lilikuwa na vipande mbili vya mawe, ambapo sheria za Mungu ziliandikwa. Wakati hekalu la Mungu lilifunguliwa mbinguni, sanduku ya agano lake ilionekana. Ndani ya Pahali patakatifu pa patakatifu mno mbinguni, sheria ya Mungu inatunzwa--sheria iliyosemwa na Mungu na kuandikwa kwa kidole chake juu ya vipande mbili vya mawe.TSHM 209.2

    Wale waliopata kufahamu maana yake waliona, zaidi kuliko mbele, nguvu za maneno ya Mwokozi: “Hata mbingu na inchi zitakapoondoka, yodi moja wala nukta moja haitaondoka.” Matayo 5:18. Sheria ya Mungu, ambayo ni ufunuo wa mapenzi yake, andiko la tabia yake, inapaswa kudumu milele.TSHM 209.3

    Katika orodha ya Amri kumi kunakuwa amri ya Sabato. Roho ya Mungu ikaonyesha wale wanafunzi wa Neno lake lile kwamba walivunja kwa ujinga amri hii kwa kutojali siku ya pumziko ya Muumba. Wakaanza kuchunguza sababu ya kushika siku ya kwanza ya juma. Hawakuweza kupata ushahidi wo wote kwamba amri ya ine iliondolewa mbali wala kwamba Sabato iligeuzwa. Wakatafuta kwa uaminifu kujua na kutenda mapenzi ya Mungu; sasa wakaonyesha uaminifu wao kwa Mungu kwa kushika Sabato yake takatifu.TSHM 209.4

    Nguvu mingi ilifanywa kwa kuangusha imani ya waamini wa Adventiste. Hakuna mtu aliweza kushindwa kuona kwamba ukubali ule wa kweli juu ya Pahali patakatifu pa mbinguni unahusika na haki za sheria ya Mungu na Sabato ya amri ya ine. Hapa kulikuwa na siri ya upinzani uliokusudiwa juu ya maelezo wazi ya umoja wa Maandiko yanayofunua huduma ya Kristo ndani ya Pahali patakatifu pa mbinguni. Watu wakatafuta kufunga mlango ambao Mungu alifungua, na kufungua mlango ambao aliufunga. Lakini Kristo alifungua mlango wa huduma ya Pahali patakatifu pa patakatifu. Amri ya ine ilikuwa ndani katika sheria iliyotunzwa pale.TSHM 209.5

    Wale waliokubali nuru juu ya upatanisho wa Kristo na sheria ya Mungu wakaona kwamba haya yalikuwa kweli ya Ufunuo 14, ambayo ni onyo la mara tatu kwa kutayarisha wakaaji wa dunia kwa ajili ya kuja kwa Bwana mara ya pili. (Tazama mwisho wa kitabu, Nyongezo). Tangazo “Saa ya hukumu yake imekuja “linatangaza kweli ambayo inapaswa kutangazwa hata upatanisho wa Mwokozi utakapoisha na atarudi kuchukua watu wake kwake mwenyewe. Hukumu ambayo ilianza katika mwaka 1844 inapaswa kuendelea hata kesi za wote zinapokwisha kukatwa, wote wahai na waliokufa; kwa sababu hiyo itaenea hata kwa kufungwa kwa rehema ya wanadamu.TSHM 210.1

    Ili watu waweze kujitayarisha kusimama katika hukumu, ujumbe unawaagiza kuogopa Mungu, na kumutukuza,” na kumwabudu yeye aliyefanya mbingu, na dunia na bahari na chemchemi za maji.” Matokeo ya kukubali kwa ujumbe huu wa malaika watatu unatolewa: “Hapa ni uvumilivu wa watakatifu wanaoshika amri za Mungu, na imani ya Yesu.” Ufunuo 14:7,12.TSHM 210.2

    Kwa kujitayarisha kwa hukumu, watu wanapashwa kushika sheria ya Mungu, kipimo cha tabia katika hukumu. Paulo anasema: “Wote waliokosa wakiwa na sheria, watahukumiwa kwa sheria, ... katika siku ile Mungu atakapohukumu siri za watu ... kwa Yesu Kristo.” “Wale wanaotenda sheria watakaohesabiwa haki.” Imani ina maana sana ili kushika sheria ya Mungu; kwani “pasipo imani haiwezekani kumupendeza.” “Kila tendo lisilotoka katika imani ni zambi.” Waroma 2:12-16; Waebrania 11:6; Waroma 14:23.TSHM 210.3

    Malaika wa kwanza aliita watu kwa “kuogopa Mungu, na kumutukuza” na kumwabudu yeye aliyefanya mbingu na dunia. Kwa kufanya hii, wanapaswa kutii sheria yake. Bila kutii hakuna ibada inayoweza kupendeza Mungu. “Kwa maana kupenda Mungu ni kushika amri zake.” 1 Yoane 5:3; Tazama Mezali 28:9.TSHM 210.4

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents