Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents
Tangu Sasa Hata Milele - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    Kujiunga Pamoja na Walimwengu

    Makanisa mengi ya kiprotestanti yamefuata mfano wa uhusiano pamoja na “wafalme wa dunia” makanisa ya taifa, kwa uhusiano wao na serkali; na makanisa mengine, kwa kutafuta mapendeleo ya dunia. Neno “Babeli” machafuko--linaweza kutumiwa kwa makundi haya yanayojidai kwamba yalipata mafundisho yao kutoka kwa Biblia, lakini yamegawanyika katika makundi isiyohesabika pamoja na kanuni ya imani za mbalimbali.TSHM 184.4

    Kazi ya kanisa la kikatolika la Roma inabisha kwamba “kama kanisa la Roma lingekuwa na kosa ya ibada ya sanamu katika uhusiano kwa watakatifu, binti yake, kanisa la Uingereza, linakuwa na kosa ya namna moja, kwa sababu lina makanisa kumi inayojiweka wakfu kwa Maria kwa namna moja linalojiweka wakfu kwa Kristo.”TSHM 184.5

    Na Dr. Hopkin husema: “Hakuna sababu ya kufikiri kwamba roho na kanuni za mpinga kristo na vitendo kusongwa kwa ile ambayo inaitwa sasa Kanisa la Roma. Makanisa ya Kiprotestanti yanakuwa na umpinga kristo ndani yao, na yanakuwa mbali kabisa ya matengenezo kwa ... maovu na ubaya.”TSHM 185.1

    Juu ya Kanisa la Presbyteria kujitenga kwa Roma, Dr. Guthrie anaandika: “Miaka mia tatu iliyopita, kanisa letu, pamoja na Biblia iliyofunguliwa kwa mwenge yake, na maneno haya maalum: “Tafuteni maandiko” kwa mabendera yake, lilitoka kwa milango ya Roma. Ndipo akauliza swali hili la muhimu: Je, waligeuka kuwa safi walipotoka kwa Babeli ? ”TSHM 185.2

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents