Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents
Tangu Sasa Hata Milele - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    Kumbusho ya Kusulubiwa

    Ukumbusho moja peke unaodumu: Mkombozi wetu atachukua hata milele alama za kusulubiwa kwake, alama pekee za kazi ya ukali ambazo zambi imetenda. Katika miaka ya milele vidonda vya Kalvari vitaendelea kuonyesha sifa yake na vitatangaza uwezo wake.TSHM 329.4

    Kristo alihakikishia wanafunzi wake ya kwamba alikwenda kuandalia makao kwa ajili yao katika nyumba ya Baba yake. Lugha wala maneno ya binadamu hayatoshi kueleza zawadi ya wenye haki. Itajulikana tu kwa wale wanaoitazama. Hakuna wazo lenye mpaka linaloweza kufahamu utukufu wa Paradiso ya Mungu!TSHM 329.5

    Katika Biblia uriti wa waliokombolewa unaitwa “inchi”. Waebrania 11:14-16. Huko Mchungaji wa mbinguni ataongoza kundi lake kwa chemchemi za maji ya uzima. Huko kunakuwa na vijito vyenye kutiririka, safi kama jiwe lingaalo, na pembeni yao miti yenye kutikisika inayotupa vivuli vyao kwa njia zilizotayarishwa kwa ajili ya waliokombolewa wa Bwana. Inchi kubwa tambarere zinainuka kuwa vilima vya uzuri, na milima ya Mungu inapandisha vilele vyao virefu. Katika inchi tambarare hizo za amani, pembeni ya vijito hivyo vya uzima, watu wa Mungu, waliokuwa wasafiri na wanaohangaika watapata makao.TSHM 329.6

    “Nao watajenga nyumba, na kukaa ndani yake; na watapanda mizabibu, na watakula matunda yake: hawatajenga na mtu mwingine kukaa ndani yake; hawatapanda, na mtu mwingine kula matunda yake: ... Na wachaguliwa wangu watafurahia kazi ya mikono yao”. “Jangwa na inchi kavu zitafurahi; na jangwa litashangilia na kutoa maua kama waridi”. “Na imbwa mwitu atakaa pamoja na mwana-kondoo, na chui atalala chini pamoja na mwana-mbuzi; na mtoto mudogo atawaongoza... Hawataumiza wala kuharibu wote katika mulima wangu wote mtakatifu”. Isaya 65:21, 22; 35:1; 11:6,9.TSHM 330.1

    Maumivu hayawezi kuwako mbinguni. Hakutakuwa na machozi tena, Hakutakuwa tena mafuatano ya maziko. “Wala mauti haitakuwa tena; wala maombolezo, wala kilio: ... kwa maana maneno ya kwanza yamekwisha kupita”. “Wala hapana mwenyeji atakayesema, mimi ni mgonjwa; watu wanaokaa ndani yake watasamehewa uovu wao”. Ufunuo 21:4; Isaya 33:24.TSHM 330.2

    Huko ni Yerusalema Mpya, muji mkubwa wa inchi mpya yenye utukufu. “Mwangaza wake ulikuwa mfano wa jiwe la bei kubwa, kama jiwe la yaspi, safi kama bilauri”. “Na mataifa ya waliookolewa watatembea katika nuru yake. Na wafalme wa dunia wataleta utukufu na heshima yao ndani yake”. “Tazama hema ya Mungu ni pamoja na watu, naye atakaa pamoja nao, nao watakuwa watu wake, na Mungu mwenyewe atakuwa pamoja nao, na atakuwa Mungu wao”. Ufunuo 21:11,24,3.TSHM 330.3

    Ndani ya Muji wa Mungu “wala hautakuwa usiku tena”. Ufunuo 22:5. Hautakuwa kuchoka tena. Tutaona ubaridi daima wa asubui bila mwisho wake. Nuru ya jua itatanguliwa na mwangaza wa ajabu ambao si wa kuumiza, lakini ambao unapita mbali sana mwangaza wa wakati wa saa sita yetu. Waliookolewa watatembea katika utukufu wa siku zote.TSHM 330.4

    “Nami sikuona hekalu ndani yake, kwa maana Bwana Mungu Mwenyezi na Mwana-Kondoo ndio hekalu lake”. Ufunuo 21:22. Watu wa Mungu wanakuwa na ruhusa ya kuendelea kuwa na umoja wazi na Baba na Mwana. Sasa tunaangalia mufano wa Mungu kama katika kioo, lakini ndipo tutamwona uso kwa uso, pasipo pazia ya giza katikati.TSHM 330.5

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents