Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents
Tangu Sasa Hata Milele - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    Namna Sabato Ilivyogeuzwa

    Unabii ulitangaza kwamba Kanisa la Kiroma “litafikiri kugeuza nyakati na sheria”. Danieli 7:25. Kwa kutoa badala kwa ibada ya sanamu, ibada ya masura sanamu na masalio kumbukumbu, jambo hilo likaingizwa kidogo kidogo katika ibada ya Kikristo. Agizo la baraza la kawaida (Tazama mwisho wa kitabu (Nyongezo)) mwishowe likaanzisha ibada hii ya sanamu. Roma ikasubutu kufutia mbali amri ya pili ya sheria ya Mungu, inayokataza ibada ya sanamu, na kugawanya amri ya kumi ili kulinda hesabu.TSHM 15.2

    Waongozi wasiotakaswa wa kanisa wakageuza amri ya ine vile vile, kwa kutangua Sabato ya zamani, siku ambayo Mungu alibariki na kutakasa (Mwanzo 2:2,3) na mahali pake wakatukuza siku kuu iliyolazimishwa na wapagani kama “siku tukufu ya jua”. Katika karne za kwanza Sabato ya kweli ilishikwa na Wakristo wote, lakini Shetani akatumika kwa kuleta kusudi lake. Siku ya jua (siku ya kwanza) (Dimanche) ikafanywa kuwa siku kuu kwa ajili ya ufufuko wa Kristo. Huduma za dini zilifanyika kwa siku hiyo, lakini ilizaniwa kama siku ya pumziko, Sabato ikaendelea kushikwa na utakatifu.TSHM 15.3

    Shetani akaongoza Wayahudi, kabla ya kuja kwa Kristo mara ya kwanza, kulemeza Sabato kwa lazimisho makali, kuifanya kuwa mzigo. Sasa, kwa kutumia nuru ya uongo ambamo alilete sabato kutazamiwa, akaitupia zarau kama sheria ya “Wayahudi”. Wakati Wakristo kwa kawaida waliendelea kushika siku ya kwanza (Dimanche) kama siku kuu ya shangwe, akawaongoza kufanya Sabato kuwa siku ya huzuni na giza ili kuonyesha machukio kwa Kiyahudi.TSHM 15.4

    Mfalme Constantini akatoa amri kufanya Siku ya kwanza (Dimanche) siku kuu ya watu wote popote katika ufalme wa Roma (Tazama Mwisho wa Kitabu ama Nyongezo). Siku ya jua ilikuwa ikitukuzwa na watu wake wapagani na kuheshimiwa na Wakristo. Alilazimishwa kufanya hivi na maaskofu wa kanisa. Walipoongozwa na hamu ya mamlaka, waliona ya kuwa kama siku hiyo moja ilishikwa kwa wote ni kusema Wakristo na wapagani, ingeendelesha uwezo na utukufu wa kanisa. Lakini wakati Wakristo wengi wenye kumcha Mungu walipoongozwa kuzania Siku ya kwanza (Dimanche) kama yenye kuwa na cheo cha utakatifu, waliendelea kushika Sabato ya kweli na kuitukuza katika utiifu wa amri ya ine.TSHM 16.1

    Mdanganyi mkuu hakutimiza kazi yake. Alikusudia kutumia uwezo wake kwa njia ya mjumbe wake, askofu mwenye kiburi anayejidai kuwa mjumbe wa Kristo. Mabaraza makubwa yalifanywa ambamo wakuu walikusanyika kutoka pote duniani. Karibu kila baraza Sabato iligandamizwa chini kidogo, wakati siku ya kwanza (Dimanche) ikatukuzwa. Kwa hiyo siku kuu ya wapagani mwishowe ikatukuzwa kama sheria ya Mungu, lakini sabato ya Biblia ikatangazwa kuwa kumbukumbu ya dini ya Kiyahudi na kawaida zake zikatangazwa kuwa za laana.TSHM 16.2

    Mkufuru akafaulu katika kujionyesha mwenyewe “juu ya yote yanayoitwa Mungu, ao kuabudiwa.” 2 Watesalonika 2:4. Alisubutu kugeuza amri moja tu ya sheria ya Mungu inayoonyesha Mungu wa kweli na wa uhai. Katika amri ya ine, Mungu hufunuliwa kama Muumba. Kama ukumbusho wa kazi ya kuumba, siku ya saba ikatakaswa kama siku ya pumziko la mtu, iliyokusudiwa kulinda Mungu wa uhai siku zote mbele ya akili za watu kama kitu cha ibada. Shetani hujitaidi kugeuza watu kwa utii wa sheria ya Mungu; kwa hivyo huelekeza nguvu zake zaidi sana juu ya amri ile inayoonyesha Mungu kama Muumba.TSHM 16.3

    Waprotestanti sasa wanalazimisha kwamba ufufuo wa Kristo Siku ya Kwanza (Dimanche) uliifanya kuwa Sabato ya Kikristo. Lakini hapana heshima ya namna hiyo iliyotolewa kwa siku ile na Kristo au mitume wake. Kawaida ya Siku ya Kwanza (Dimanche) ilikuwa na asili yake katika ile “siri ya uasi” (2 Watesalonika 2:7), ambayo, hata katika siku ya Paulo, ilianza kazi yake. Sababu gani inayoweza kutolewa kwa mageuzi ambayo Maandiko hayakuruhusu?TSHM 16.4

    Katika karne ya sita, askofu wa Roma alitangazwa kuwa kichwa cha kanisa yote nzima. Dini ya kipagani ikatoa nafasi kwa kanisa la Roma. Joka akamupa nyama “nguvu zake”, na kiti chake cha ufalme na mamlaka nyingi”. Ufunuo 13:2 (Tazama Nyongezo).TSHM 16.5

    Sasa ikaanza miaka 1260 ya mateso ya Papa iliyotabiriwa katika mambo ya unabii wa Danieli na Ufunuo. Danieli 7:25; Ufunuo 13:5-7. Wakristo walilazimishwa kuchagua au kuacha uaminifu wao na kukubali huduma na ibada za Papa, au kutoa maisha yao katika gereza, au kuuawa. Sasa maneno ya Yesu yalitimilika: “Nanyi mutatolewa hata na wazazi wenu, na ndugu, na jamaa, na rafiki, na wengine wenu watawaua. Na mutachukiwa na watu wote kwa ajili ya jina langu” Luka 21:16, 17.TSHM 17.1

    Ulimwengu ukawa shamba kubwa sana la vita. Kwa mamia ya miaka kanisa la Kristo lilipaswa kuishi katika maficho na giza. “Yule mwanamuke akakimbia hata pori; kule ana pahali palipotengenezwa na Mungu ili wamulishe kule siku elfu moja mia mbili na makumi sita” Ufunuo 12:6.TSHM 17.2

    Kutawazwa kwa utawala wa Kanisa la Roma kulionyesha mwanzo wa miaka ya giza. Imani ikahamishwa kutoka kwa Kristo na kwenda kwa Papa wa Roma. Badala ya kutumainia Mwana wa Mungu kwa ajili ya musamaha wa zambi na wokovu wa milele, watu wakatazamia Papa, na mapadri ambao aliwatolea mamlaka yake. Papa alikuwa mpatanishi wao wa kidunia. Alisimama kwa mahali pa Mungu kwa ajili yao. Kwenda pembeni ya mapenzi yake ilikuwa sababu ya kutosha kwa azabu kali. Kwa hiyo akili za watu zikatoka kwa Mungu zikageukia watu wapotevu, wabaya, niseme nini tena, kwa mfalme wa giza anayetumia uwezo wake kupita wao. Wakati Maandiko yanapokomeshwa na mtu anapojiona mwenyewe kuwa kama mkubwa kabisa, kitu kitakacho tazamiwa tu ni hila, madanganyo, na upunguo wa tabia njema.TSHM 17.3

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents