Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents
Tangu Sasa Hata Milele - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    Katika Inchi Mbalimbali kwa Wakati Moja

    Kama Matengenezo ya karne ya kumi na sita, Mwendo (kazi), la Kuja kwa Yesu likaonekana katika inchi mbalimbali kwa wakati moja. Watu wa imani wakaongozwa kujifunza mambo ya unabii na wakaona ushuhuda wa kusadikisha kwamba mwisho ulikuwa karibu. Makundi mbali mbali ya Wakristo, kwa kujifunza Maandiko tu, wakafikia kwa kuamini kwamba kuja kwa Mwokozi kulikuwa karibu.TSHM 171.1

    Miaka mitatu baada ya Miller kufikia kwa maelezo yake ya mambo ya unabii. Dr. Joseph Wolff, “Mjumbe kwa ulimwengu,” akaanza kutangaza kukaribia kwa kuja kwa Bwana. Alizaliwa katika Ujeremani, wazazi wake Wayahudi. Alikuwa Kijana sana wakati ule, akasadikishwa kwa habari ya kweli ya dini ya kikristo. Alikuwa msikizi mwenye bidii sana kwa mazungumzo katika nyumba ya baba yake mahali Wayahudi waaminifu walikuwa wakikusanyika kila siku kwa kuzungumzia matumaini ya watu wao, utukufu wa kuja kwa Masiya, na kuimarishwa tena kwa Israeli. Siku moja, kusikia Yesu wa Nazareti kutajwa, kijana akauliza kujua alikuwa nani. “Muyahudi wa talanta kubwa mno” wakajibu” Lakini alipojidai kuwa Masiya, baraza la hukumu la Wayahudi likamkatia hukumu ya kifo.”TSHM 171.2

    “Sababu gani,” akafuatisha mwenye kuuliza, “je, Yerusalema iliharibiwa, na sababu gani tunakuwa katika utumwa?”TSHM 171.3

    “Ole, ole,” akajibu baba yake, “kwa sababu Wayahudi waliua manabii.” Mara moja wazo likaja moyoni mwa mtoto: “Pengine Yesu pia alikuwa vilevile nabii, na Wayahudi wakamuua wakati alikuwa bila kosa.” Ingawa alikatazwa kuingia katika kanisa la Kikristo, akakawia mara kwa mara inje kusikiliza mahubiri. Alipokuwa na miaka saba tu ya kuzaliwa, alikuwa akijisifu kwa jirani wake mkristo juu ya kushinda kwa Israel wakati ujao wa kuja kwa Masiya. Mzee akasema kwa upole: “Kijana mpenzi, nitakwambia nani aliyekuwa Masiya wa kweli: alikuwa Yesu wa Nazareti,... ambaye wababu wako walimsulubisha... Wende nyumbani na usome sura ya makumi tano na tatu ya Isaya, na utasadikishwa kwamba Kristo ni Mwana wa Mungu.”TSHM 171.4

    Akaenda nyumbani na akasoma Maandiko. Kwa ukamilifu wa namna gani ilitimilika kwa Yesu wa Nazareti. Je, maneno ya mkristo yule ni ya haki? Kijana akauliza baba yake maelezo ya unabii lakini akakutana na ukimya bila huruma na hakusubutu tena kamwe kusema inayoelekea fundisho lile pamoja naye.TSHM 171.5

    Wakati alipokuwa na miaka kumi na moja tu ya kuzaliwa, akaenda duniani kupata elimu, kuchagua dini yake na kazi yake ya maisha. Peke yake na bila senti hata moja, alipashwa kutafuta njia yeye mwenyewe. Akajifunza kwa bidii, na kujisaidia mwenyewe kwa mahitaji yake kwa kufundisha Kiebrania. Akaongozwa kukubali imani ya dini ya Roma na akaenda kufuata mafundisho yake katika College ya “Propagande de la Foi” (kutangaza imani). Hapo akashambulia kwa wazi matumizi mabaya ya kanisa na akalazimisha matengenezo. Baada ya mda, akatoshwa. Ikawa wazi kwamba hakuweza kamwe kuletwa kwa kutii utumwa wa dini ya Roma. Akatangazwa kuwa mtu asiyeweza kusahihshwa na kuachwa kwenda mahali palipompendeza. Akaenda Uingereza na akajiunga na kanisa la Uingereza. Baada ya miaka miwili ya majifunzo akaanza kazi yake mwaka 1821.TSHM 171.6

    Wolff aliona kwamba mambo ya unabii hutangaza kuja kwa Kristo mara ya pili kwa nguvu na utukufu. Alipotafuta kuongoza watu wake kwa Yesu wa Nazareti kama Ni yule aliyeahidiwa, kuwaonyesha kuja kwake kwa mara ya kwanza kama kafara kwa ajili ya zambi, akawafundisha pia juu ya kuja kwake kwa mara ya pili.TSHM 172.1

    Wolff aliamini kuja kwa Bwana kuwa karibu. Maelezo yake ya nyakati za unabii yakamfanya kuzania kurudi huko kama tarehe iliyoonyeshwa na Miller. “Je, Bwana wetu ... hakututolea ishara za wakati, kusudi tupate kujua hata, kukaribia kwa kuja kwake, jinsi mmoja anavyojua kukaribia kwa wakati wa jua kali kwa mtini na kutoa majani yake? Inatosha ... itajulikana kwa ishara za wakati, kwa kutushawishi kujitayarisha kwa ajili ya kuja kwake, kama vile Noa alivyotayarisha safina.”TSHM 172.2

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents