Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents
Tangu Sasa Hata Milele - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    32 / NAMNA YA KUMSHINDA SHETANI

    Vita kuu kati ya Kristo na Shetani ni karibu kuisha, na mwovu huyo anazidisha mara mbili juhudi zake kwa kuvunja kazi ya Kristo kwa ajili ya mtu. Kwa kushikilia watu katika giza na ugumu wa moyo hata upatanishi wa Mwokozi umalizika ndiyo shabaha anayoitafuta kutimiza. Wakati ubaridi unapokuwa mwingi ndani ya kanisa, Shetani hajali. Lakini wakati roho zinapochunguza, “Nifanye nini nipate kuokolewa?” anakuwa pale kupiganisha uwezo wake kupinga Kristo pia na kupinga mvuto wa Roho Mtakatifu.TSHM 253.1

    Kwa wakati moja wakati malaika walipokuja kujionyesha wao wenyewe mbele ya Bwana, Shetani akakuja vilevile miongoni mwao, si kwa ajili ya kuinama mbele ya Mfalme wa Milele, lakini kuharakisha makusudi yake maovu ya kushindana na wenye haki. Utazame Yobu 1:6. Yeye anahuzuria wakati watu wanapoabudu, kutumika kwa juhudi kutawala mawazo ya wanaoabudu. Kwa namna anavyoona mjumbe wa Mungu kutafuta Maandiko, anaandika yote juu ya fundisho litakalofundishwa. Ndipo anatumia werevu wake na akili ili habari isiweze kufikia wale ambao anawadanganya kwa jambo halisi lile. Yule anayehitaji onyo zaidi atashurutishwa katika kazi ya jambo fulani ao kwa njia ingine atapata kizuizi kwa kusikia neno.TSHM 253.2

    Shetani anaona watumishi wa Mungu wakilemewa kwa sababu ya giza inayofunika watu. Anasikia maombi yao kwa ajili ya neema ya Mungu na uwezo kwa kuvunja mvuto wa ubaridi na uvivu. Halafu kwa nguvu mpya anajaribu watu kwa anasa ya tamaa ao kujifurahisha, na kwa hivyo anaua akili zao ili washindwe kusikia mambo kabisa wanayohitaji zaidi kujifunza.TSHM 253.3

    Shetani anajua kwamba wote wanaozarau maombi na Maandiko watashindwa kwa mashambulio yake. Kwa hiyo anavumbua kila kitu cha kuvuta moyo. Wasaidizi wake wa mkono wa kuume wanakuwa na juhudi siku zote wakati Mungu anakuwa kwa kazi. Wataonyesha watumishi wa kweli wa Kristo wenye kujikana kama wanaodanganywa ao wanaodanganya. Ni kazi yao kusingizia makusudi ya kila tendo bora, kueneza mambo ya kuchongea, na kuamsha mashaka katika mioyo ya wajinga. Lakini inaweza kuonekana upesi wanakuwa watoto wa nani, ambao mfano ni wa nani wanaoufuata, na wanafanya kazi ya nani. “Mutawatambua kwa njia ya matunda yao.” Matayo 7:16; utazame vilevile Ufunuo 12:10.TSHM 253.4

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents