Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents
Tangu Sasa Hata Milele - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    14 / UKWELI UNAENDELEA KATIKA UINGEREZA

    Wakati Luther alipokuwa akifungua Biblia iliyofungwa kwa watu wa Ujeremamy, Tyndale akasukumwa na Roho wa Mungu kufanya tendo lilelile katika Uingereza. Biblia ya Wycliffe ilitafsiriwa kutoka kwa Kilatini, ambamo mulikuwa makosa mengi. Bei ya kurasa zilizoandikwa ilikuwa juu sana na kwa hiyo mtawanyiko wake ulikuwa wa shida.TSHM 114.1

    Kwa mwaka 1516, kwa mara ya kwanza Agano Jipya likachapwa katika lugha ya asili ya Kigiriki. Makosa mengi ya tafsiri ya kwanza yakasahihishwa, na maana yakarudishwa vizuri zaidi. Nakala zile zikaletea watu waliojifunza ufahamu bora kwa kweli na zikatoa mwendo mpya kwa kazi ya matengenezo. Lakini sehemu kubwa ya watu walikosa Neno la Mungu. Tyndale alipaswa kutimiza kazi ya Wycliffe katika kutoa Biblia kwa watu wa inchi yake.TSHM 114.2

    Akahubiri bila woga mambo ya hakika yake. Kwa tangazo la Papa kwamba ni kanisa lililotoa Biblia, na ni kanisa pekee linaloweza kuieleza, Tyndale akajibu: “Kamwe haukutupatia Maandiko, ni wewe uliyeyaficha kwetu; ni wewe uliyewachoma wale walioyafundisha, na kama ungaliweza, ungalichoma Maandiko yenyewe.”TSHM 114.3

    Mahubiri ya Tyndale yakaamsha usikizi kubwa. Lakini mapadri wakajitahidi kuharibu kazi yake. “Ni kitu gani kinapaswa kufanywa?” akapaza sauti. “Siwezi kuwa po pote. Ee! kama Wakristo wangalikuwa na Maandiko matakatifu katika lugha yao wenyewe, wangaliweza wao wenyewe kushindana na wenye kutumia maneno madanganyifu hawa. Bila Biblia haiwezekani kuimarisha watu katika kweli.”TSHM 114.4

    Nia mpya ikaja katika mawazo yake. “Injili haitasema lugha ya Ungereza miongoni mwetu? ... Kanisa linapaswa kuwa na nuru ndogo kwa wakati wa azuhuri kuliko wakati wa mapambazuko yake? ... Wakristo wanapashwa kusoma Agano Jipya katika lugha yao ya kuzaliwa.” Ila tu kwa njia ya Biblia watu waliweza kufikia ukweli.TSHM 114.5

    Mtaalamu mmoja wa Katoliki katika mabishano pamoja naye akapaza sauti ya mshangao, “Ingekuwa vema kutokuwa na sheria za Mungu kuliko kukosa zile za Papa.” Tyndale akajibu, “Ninazarau Papa na sheria zake zote; na kama Mungu angenipatia maisha, kabla ya miaka mingi nitawezesha kijana anayeongoza jembe la kukokotwa na ngombe kufahamu Maandiko zaidi kuliko ninyi.”TSHM 114.6

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents